Close

JE NI SAHIHI KUFANYA IBADA KATIKA KANISA LENYE KABURI NDANI YAKE?

[ad_1]

Kama nilivyokwisha elezea katika makala ya Nabii Hebron yaliyopita, nilishaelezea ni kwa nini Petro (yule mtume wa YESU) alivyouliwa alizikwa ndani ya kanisa. Ile ina maana hii; Petro yuko na YESU wa kweli, yeye amezikwa asiandike tena katika nyakati hizo na ndiyo sababu Injili ya kweli ilifungwa na injili ya uongo ilisambaa zaidi hata sasa.
Katika kanisa pale ni mahali patakatifu, siyo mahali pa kuwekwa mizoga au hata kuhifadhiwa mafuvu au mifupa ya watu waliokufa. Kila mtu hata kimwili hapendi kukaa kaburini, ni sababu kaburi na mahali pa mateso, pabaya natumaini hata wewe ambaye unajua siku moja utakufa ukaweka ndani ya moyo wako haufurahii kufukiwa kaburini. Sasa tukija kiroho na ki-formula za MUNGU, kanisani ni mahali pake yeye, na siyo mahali pa kuwawekea wafu au kuwazikia wafu. Hii ni sababu MUNGU yeye siyo MUNGU wa wafu ni MUNGU wa wenye uhai na uzima.Shetani ametumia mbinu hii kuwateka watu na hata imani zao pasipo kujua japo wanaamini ni madhabahu hizo wasijue kuwa wao wanaabudu mungu wa wafu au mungu mfu, na hii unaposhiriki tu katika nyumba ya ibada ambayo watu huzikwa ndani, au wanyama, uelewe hapo unajipotezea muda wako, haupo na MUNGU aliye hai, bado upo katika himaya ya mungu mfu, hivyo kama ni ukristo wako au na mwingine ukristo huo ni mfu mbele za MUNGU wa mbinguni, wala sio ukristo hai sababu YESU yu hai, yupo mbinguni, tunamwabudu aliye hai, na kama upo katika madhabahu hiyo uelewe wewe ni mkristo mfu, YESU aliye hai anasema huu ndio wakati wake, hakuna nyakati nyingine zaidi hata katika Biblia. Sasa tunasubiri unyakuo, aliponieleza YESU habari hizi akaniambia, uwaeleze mataifa yote wajue ukweli na watakaosikia wataponywa.
Hii yote ni kazi ya mpinga kristo, amelifanya kanisa ni kaburi. Hata mimi YESU sikuzikwa katika madhabahu. Na ukiona madhabahu imezikwa mtu ndani ya kanisa, madhabahu hiyo ni mfu na inaunganisha na matawi yake yote. Alinieleza maneno haya akitoa machozi kwa ajili ya upendo alio nao kwa watu, na wanapotezwa watu wengi wakijua wapo na MUNGU wa hao kumbe mungu mfu. YESU amesalitiwa na watumishi baadhi yao katika ulimwengu, na alishasema mtawatambua kwa matunda yao. Rejea sasa kwa YESU anakupenda na uokoke umrudie tena. Ndiyo sababu roho ya mauti ina uhalali wa kuishi ndani yako na mateso.
Sema BWANA YESU, naomba unisamehe, dhambi zangu zote nilizozifanya kwa kujua, na kutokujua, niliabudu katika kanisa lenye kaburi ndani, nikawa mfu, naomba unifufue sasa, unishike mkono nisipotee tena, uniongoze. Amen.
Zaidi tembelea website www.prophethebron.org

Nabii Hebron.

[ad_2]