Close

JE UNAJUA BAADA YA HUKUMU WENYE DHAMBI WATANYAKULIWA NA MWANAKONDOO WA JOKA KUU?

[ad_1]

Leo tena ni shule nyingine ambayo napenda kufundisha juu ya nini kitatokea baada ya mwana kondoo wa MUNGU aliye hai atakaohukumu ulimwengu katika mara ya pili ya ujio wake akiwa pamoja na wale watakatifu waliopo mbinguni 144,000. Sasa baada ya watu kuhukumiwa na yeye joka kuu pia alishatengeneza serikali yake akaiga kama vile management ya mbinguni ilivyo. Katika serikali ya kuzimu, joka kuu ndiye mungu wao mkubwa na shetani yeye anaitwa mwana kondoo wa joka kuu na wale 144,000 ni wale watu ambao walikufaga zamani hizo walikuwa wakatili mfano Farao, kina Herode na wengineo hao wataunganika na mwana kondoo wa joka kuu kuja kuwalaki wenye dhambi na kuungana nao katika ufalme wa jehanamu kupata  walichokipanda. Na hata sasa hawa wachawi na manabii wa uongo walikuwa wanasaidiwa na serikali ya joka kuu, ila sasa mambo ni magumu aliniagiza YESU na mimi akiwepo malaika mkuu Mikaeli na jeshi lake, nilimfunga huyu mungu wao na kuharibu kazi zake hata sasa kuzimu inajua  na umoja wa wachawi wanajua, mungu wao ambao ndie joka kuu sasa hawamuoni.         
Ninawasihi wanadamu sasa hivi ulimwengu hausemi ukweli kuhusu YESU wala habari za MUNGU ipasavyo 98% ni chukizo mbele za MUNGU, siyo habari nzuri imekuwa ni habari mbaya, kataa habari mbaya ili usije ukalakiwa na wewe na mwana kondoo wa joka kuu ambaye ndiye shetani na ndiye mpinga kristo.
Hivi umeshajiuliza swali je? YESU ni kondoo mnyama kweli? Jibu yeye siyo mnyama. Sasa umeshajiuliza kwa nini makanisa baadhi wanachora picha za kondoo kanisani au hata katika majoho? Pata siri uelewe sasa, picha yeyote unayoona katika kanisa au majoho huyo ndiye huyo mwana kondoo wa joka kuu ambaye yeye ameandaliwa ili baada ya hukumu na serikali yake awalaki wenye dhambi. Mfunguke ufahamu hiyo picha ndiyo maana yake. YESU siyo kondoo mnyama. Ile neno kondoo imetumika kama sadaka ambayo yeye YESU alijitoa kwa MUNGU ili damu yake imwagike watu wapone. Ila cha ajabu makanisa badala ya kufuata neno lilivyo sasa yamechukua picha ya kondoo na kondoo huyo kila mahali ilipo picha yake, uelewe ipo roho ya mwana kondoo wa joka kuu hapo sipo pa mwana kondoo wa MUNGU aliye hai.
Pili katika nyumba ya sala haitakiwi iwe na sanamu yeyote ile, sasa huyo kondoo siyo sanamu? Mtoto wa MUNGU zaidi endelea kusoma makala ya Nabii Hebron utajifunza mengi, na utamjua YESU WA NAZARETI.
Na zaidi nawakaribisha watu wote wa mataifa yote mje mjifunze ukweli alionifundisha mimi ili niukomboe ulimwengu kutoka katika mikono ya shetani ili watu wapone roho zao na niwaombee tena pasipo malipo yeyote maana yeye hutoa bure, ukikuta unachajiwa pesa hata kama ni mtumishi anataja jina la YESU uelewe ndani yake YESU hayupo ni mapepo na roho ya mpinga kristo.

NABII HEBRON.

[ad_2]