Close

JE UNAJUA NJIA YA JEHANAMU ILIVYO?


Ufunuo Wa Yohana 21:27
Watoto wa MUNGU nawasalimu kwa jina la YESU KRISTO WA NAZARETI ambaye lengo lake yeye kuja ulimwenguni ni kututoa katika njia ya jehanamu na tumfuate yeye katika njia ya mbinguni. Nitaelezea kuhusu njia ya jehanamu uijue nitaelezea kimwili pia na kiroho. Njia hii ya jehanamu kiongozi wake ni yesu kristo wa uongo anaitwa wa uongo sababu ili amteke mtu silaha yake kubwa ni kumpa mwanadamu elimu ya uongo kwa kulibadilisha neno la MUNGU, na kuvunja amri za MUNGU.
1.     KIMWILI
Njia hii ya jehanamu kwanza kabisa ni pale unapoona mtu anatenda dhambi, anapoyatenda hayo yafuatayo nitaelezea haijalishi ameokoka au yeye ni mkristo hewa.
Kufanya uzinzi, ulevi, kuabudu sanamu, kuwa na wivu, chuki, kuvuta bhangi, sigara, madawa ya kulevya, kwenda disko, kucheza na kuimbe miziki ya kidunia, kusema uongo, kuoa wake zaidi ya mmoja, uwizi na matendo yote ya ufisadi (endapo unayefanya hayo uelewe upo katika njia ya jehanamu siyo ya mbinguni haijalishi unasema unaenda mbinguni) je hayo unayofanya ni matendo ya mbinguni? Jibu siyo.
2.     KIROHO
Haya nitakayoyataja ni baadhi tu ambayo yatakupa picha ujielewe katika roho je upo salama au tayari kiroho upo jehanamu na umeishikilia njia yake kwenda motoni. Kwanza kabisa hakikisha kuhani wako ni kweli MUNGU ndiye kamleta, kama amejiita au ni mchungaji wa mshara uelewe roho zenu zinapelekwa katika njia pana ya jehanamu katika ulimwengu wa roho , kuabudu sanamu, misalaba, ibada za wafu, ubatizo wa kikombe, maji ya kisima, kubatizwa kwa jina la mchungaji, kubatizwa ukiwa mtoto mdogo, kushiriki katika kanisa lolote lile ambalo linachangisha pesa kanisani au mahali popote pale, imeandikwa nyumba ya MUNGU ni nyumba ya sala, sasa ikiwa ni kinyume elewa hapo siyo mahali pa njia ya mbinguni, hapo ni mahali pa njia ya jehanamu katika ulimwengu wa roho, na uelewe pia ili uende mbinguni ni lazima katika uliwmengu wa roho uyafuate yale ya kweli tu katika biblia na siyo kinyume au kuchanganya uongo na ukweli hapana.
Kanisa lenye huduma sita zadala ya zile tano tu alizozianzisha YESU hapo pana njia ya jehanamu, huduma hii ya sita inaitwa Askofu, ukiona kiongozi wa kanisa amevaa kofia akihubiri ujue anawapeleka watu katika njia ya jehanamu. Zaidi soma makala ya Nabii Hebron Tanzania, nimeelezea mengi alivyonifundisha YESU ili niwafungue watoto wake macho na fahamu zao wapone roho zao sababu wengi mno wanapotezwa badala ya kuwekwa katika njia ya mbinguni sasa katika ulimwengu wa roho wameishika njia ya jehanamu. Japo na waumini hawapendi kwenda jehanamu, wanaongozwa na viongozi vipofu kiroho na kuwafanya waumini nao wawe vipofu wasimuone MUNGU wala kufika mbinguni. Ukiongozwa na mtumishi yeyote ambaye jina lake lipo kwenye mtandao wa freemason Internet au ni mchawi au mfanya mazingaumbwe, mfufua misukule au yeye mwenyewe hajabatizwa ubatizo ulioko katika katiba ya MUNGU yaani biblia, au anayeongozwa na nguvu za mizimu au anayejiita yeye ni YESU au kujifananisha na MUNGU au anajiita mungu mtu au mzinzi, mlevi, anachangisha watu pesa, hawa wote wanawapeleka watu jehanamu hayo ni matendo ya shetani na biblia imekataa. Au mtumishi yeyote aliyeitwa na YESU halafu akamsaliti hapo elewa hakuna tena njia ya mbinguni, ndani yake ni yesu wa uongo amekaa hivyo yesu huyo wa uongo atawaongoza watu katika elimu ya uongo ili awadumaze roho zenu na mpofuke msione njia ya mbinguni bali mbakie katika njia ya jehanamu na ile siku ya mwisho watu watalia na kusaga meno sababu watavuna wasichotegemea badala ya paradise ni jehanamu.
Mwana wa MUNGU ulilopo katika taifa lolote simama imara leo hii hali ni mbaya huu ni wakati wa hatari, kufumba macho na kufumbua ipo siku utakuta wengine wamenyakuliwa katika unyakuo na wengine walio katika njia ya jehanamu kimwili na kiroho watabakia hapo hapo wateseke kwa muda wa miaka saba na mpinga kristo, kataa sasa mafundisho ya mpinga kristo ili usije ukabakia hapa ulimwenguni wakati wa unyakuo, watakaobakia ni wale wapinga kristo (changanya neno na uongo) na watenda dhambi, na kila mtu ambaye hajaokoka na kuzaliwa mara ya pili. Zaidi uwatumie na wengine ujumbe huu ili wasome na wafunguke na wewe utabarikiwa na YESU WA NAZARETI.
NOTE:
BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote naomba leo uniandike katika kitabu chako cha uzima wa milele unitoe katika kitabu cha njia ya jehanamu, uniongoze wewe YESU na ROHO MTAKATIFU peke yake nyie ndio kweli, shetani sikutaki na mpinga kristo sikutaki katika jina la YESU WA NAZARETI aliye hai.
NABII HEBRON.