JINSI VIONGOZI WA KANISA WALIVYOACHA KUMTUMIKIA MUNGU NA KUTAFUTA PESA.

[ad_1]

Namshukuru  MUNGU  kwa kunipa kibali cha kuandika Ujumbe huu, juu ya Viongozi wa Kanisa , kwa sababu Viongozi wamepewa  Jukumu la kusimamia  waumini ili wasipotee,  lakini cha kushangaza wameacha maagizo waliopewa na Mwanzilishi wa Kanisa ambaye ni YESU KRISTO WA NAZARETI, wakakimbilia mambo ya dunia, kama Kutafuta pesa.

Nitaeleza kuhusu kiongozi wa Kanisa ni nani?
Kiongozi wa kanisa ni Mtumishi wa MUNGU aliyechaguliwa kwa kusudi la kuongoza kanisa, ambalo ni waumini, ili watoto wa MUNGU waweze  kwenda Mbinguni.

Kiongozi wa kanisa ni pamoja na Wachungaji, Maaskofu, Wainjilisti  na Waalimu.YESU amewapa kazi ya kuwaongoza watoto wake ili waurithi ufalme wa mbinguni. Lakini sasa hivi ni kinyume. Viongozi ndio wamekuwa kisababisho cha waumini kulia, kuhangaika na kuteseka wakati baba yao aliyewaumba yupo. Wao ndio chanzo kikubwa kanisa kuteseka na waumuini wakaona kama BABA yao aliye mbinguni hayupo, sasa hivi yuko Karibu kurudi, viongozi wanaofanya mambo ya dunia watahukumiwa. Waliiacha misingi aliyoiweka YESU KRISTO WA NAZARETI na kufuata mambo ya dunia kama yafuatayo:-

  • Kuchangisha pesa  makanisani, (Harambee)
  • Kubatiza ubatizo wa beseni, ndoa za shida na Raha
  • Kufanya minada makanisani, sikukuu za Mavuno
  • Nyumba na Magari ya kifahari
  • Wamejiunga na Vyama vya Freemason.
  •  
Na ukisoma kwenye kitabu cha waraka wa kwanza kwa Timotheo 3:1-7  inaeleza kwamba Askofu au Mtumishi anatakiwa awe mtii, awe na mke mmoja, asiwe mwenye kupenda pesa, awe mpole kiasi, awe mnyenyekevu, awe mwenye kusikiliza watu, asiwe na majivuno, lakini mambo yamebadilika, kiongozi ndiye mwenye kuoa wake wengi, ndiye mwenye kufanya minada makanisani na baadhi yao wanamagari ya kifahari na hizo pesa wanazipata kwenye sadaka za waumini. Unakuta kwenye kanisa kuna sadaka nyingi wakati sadaka ni Fungu la kumi na shukurani basi, na pia ukipenda  kumtolea MUNGU kwa hiyari yako.

Viongozi wa kanisa wameacha kufundisha mambo ambayo YESU anayoyataka, wao wanafanya kinyume , viongozi wa kanisa wamejihusisha  na kuuza madawa ya kulevya, wanafungisha ndoa za mashoga, wanazini na waumini, wanatapeli watu pesa zao na magari yao, eti anakuambia njoo nikutolee unabii kumbe anataka pesa zako. Watumishi wamekuwa wachawi, washirikina kuliko hata waganga wa kienyeji, Hivi kweli ndio mambo ambayo YESU amewatuma? Jibu ni hapana.  Viongozi mnaofanya hivyo; Ole iko juu yenu sasa hivi.

Inasikitisha sana viongozi wamemuacha MUNGU na kutumia Majini Muhubiri ili kuwakamata watu walete pesa makanisani. Hii ni aibu kubwa sana. YESU hapendi kabisa na hukumu iko juu yao. Viongozi wamesabisha waumini wawe Masikini wa kiroho na kimwili, Watu wanahangaika kumtafuta YESU wa kweli lakini viongozi wanawapotosha. Viongozi wa kanisa wamesababisha waumini kutangatanga na kukosa mwelekeo.

Viongozi wamekuwa wakichangisha pesa kama vile:-
Harambee ya kujenga makanisa, kuchangisa pesa ya kufanya mikutano ya Injili, wakati wanatakiwa  hawa viongozi wamuombe MUNGU ili awaletee watu wa kujenga Makanisa na sio kuchangisha waumini,  watu wanalia tuu PESA PESA, Ibada siku hizi zimekuwa za kutiana Moyo. Unakwenda Kanisani Kuanzia January mpaka December hauoni majibu yako, Viongozi hawa wametumwa kutafuta Pesa au kuponya Roho za Watu? Siku hizi Mikutano ya injili ni kutapeli watu hamna udhihirisho wowote. Wewe mwana wa MUNGU unayesoma Makala hii ukiona michango makanisani ondoka ukamtafute YESU wa kweli hao viongozi wanatafuta pesa tuu. Mbona wao wana magari ya kifahari wakati wewe nyumbani  hata centi  hauna,  wao ndio
wanakuchuna wewe tu, funguka  ufahamu mwana wa MUNGU mbona na wewe hawakuombei ili na wewe upate vitu kama wao walivyonavyo.

Viongozi wa kanisa hawawathamini wale ambao hawana pesa wakifanya makosa huwatenga. Je? YESU aliwatenga wenye Dhambi ? Jibu ni hapana, kwanini viongozi hawawaombei ili watu watubu na wamrudie YESU.

Nyie viongozi mnaofanya hivyo sasa YESU yuko kazini, mtaona mtashushwa mapaka ziro, YESU amekasirika mmeacha kazi yake, mkaanza kutafuta Pesa badala ya kuhubiri injili. Na YESU yupo kazini sasa kuwakomboa watoto wake, amewaona wanapata shida sana, wanahangaika, na atawatoa wale viongozi wote waliomsaliti.

Viongozi  wa kanisa wamefanya nchi hii iingie  kwenye matatizo, ndio wanahujumu uchumi wa Tanzania na kuwafanya watanzania wawe maskini, kwasababu wao wanatakiwa waiombee nchi na taifa zima. Wao ndio wanatakiwa kuwaongoza  wana wa MUNGU. Wamemkasirisha MUNGU hata wakifanya mikutano ya kuombea nchi, MUNGU hawezi kuwasikiliza kwasababu hawafuati mapenzi yake na sheria zake. YESU amewakataa kabisa mpaka watubu.

YESU amekasirika amemwinua Mtumishi wake Mtume na Nabii Hebron Kuupindua ulimwengu huu uliotekwa na Shetani 98%. Na amempaka mafuta ya kuongoza ili wana wa MUNGU wamrudie YESU. Ukubali, usikubali yeye ndiye atakayewaongoza  wana wa MUNGU ili wasipotee na wasipate shida tena. MUNGU aliona hakuna ambaye anaweza kumwinua akamchagua yeye peke yake. Kwa maana viongozi wote wa kanisa wanatafuta pesa tu, hawaponyi roho za watu. Tuliona kwamba kanisani ni mahali pa kuponea kumbe ndio tunateseka na kuibiwa nyota na viongozi wa kanisa. Jiulize twende wapi? Jibu twende kwa YESU KRISTO WA NAZARETI ndio mahali sahihi Makanisa yamekuwa  hayafai kabisa ni bora ukae nyumbani, maana ukienda makanisani ni michango mingi. Unakuta ibada moja inamichango minne. Funguka mwana wa MUNGU usiibiwe tena.

Asilimia kubwa viongozi ni vipofu hawaoni kabisa wamefuata mambo ya pesa, badala ya kuwafungua wana wa MUNGU. Hii inatisha sana ukiona kiongozi mzinzi, mlevi na anafanya mambo ambayo hayampendezi MUNGU. Unakata tamaa kabisa hata ya kwenda kanisani, ni kwa sababu tu ya upofu wao, ni kweli MUNGU amewaacha kabisa, kama MUNGU angekuwa yuko nao, watu wasingepata shida maana wapo viongozi wanowaombea, badala yake wao ni kutafuta pesa. Ole,iko juu yao wanajijua na wapo tunawaona kabisa.

Ndugu msomaji wa makala hii mahali ulipo mwangalie YESU peke yake, yeye ndiye anaweza kukufundisha na kukuelekeza, watumishi siku hizi wanatafuta pesa hawana muda na wewe hata  kukuombea ufanikiwe. YESU hayupo makanisani, hawezi kuingia kwenye  mapango ya wanyang’anyi, sehemu wanazochangisha pesa. Mwenyewe  ukiangalia kwa macho ya damu na nyama walivyokuwa na utajiri na majumba ya kifahari. Hivi kweli kanisa la la YESU linaweza kuwa na mabenki, mahoteli? Jibu ni hapana. Sasa ndio utajua kweli hawamtumikii MUNGU.  Kazi yao ni kutafuta pesa.

Ndugu msomaji usirudi huko tena, ukikuta Viongozi wa kanisa wana batiza watoto Wadogo na maji ya kikombe, kubariki watu wazima, huko YESU hayupo kabisa wewe tafuta kanisa la YESU wa kweli ambalo halichangishi pesa, wala haliwaibii watu vitu vyao. Viongozi wa kanisa wamefanya tumkosee MUNGU wetu kwa kutupeleka pabaya.

Omba MUNGU akuonyeshe mahali sahihi pa kuabudu usirude tena huko . Mrudie YESU awe Bwana na mwokozi wa maisha yako.
Ubarikiwe wewe uliyesoma makala hii utafunguka utajua kweli viongozi wanatafuta pesa tu badala ya kufanya kazi ya YESU aliyowaachia.  

MWINJILISTI MARTHA IMANI

[ad_2]