Close

MAELEZO YA YOUTUBE: KICHAA APONYWA LIVE KATIKA IBADA

[ad_1]

Nabii Hebron:Hebu tulia
Ndugu wa Emmanuel:Haongei na asemi chochote
Ndugu wa Emmanuel: Anaitwa Emmanuel Njau
Nabii Hebron: Muda gani sasa?
Ndugu wa Emmanuel: kama siku tatu hivi
Nabii Hebron: Huyu wamemlipua aisee, sawa?!
Nabii Hebron: Sasa ngoja niuzime huu moto. sawa sawa?
Nabii Hebron: Anaitwa nani?
Ndugu wa Emmanuel: Anaitwa Emmanuel
Nabii Hebron: Emmanuel niangalie
Nabii Hebron: Niangalie
Nabii Hebron: Huyu wamemlipua. Sawa?!
Nabii Hebron: Na wewe uliyemlipua muachie haraka. Muachie Emmanuel.Emmanuel nakuchomoa kwenye kichaa, na nyota narudisha na nafsi, njooooo…
Nabii Hebron: Niwekeeni pale basi.
Nabii Hebron: Askofu fanya kazi.
Nabii Hebron: Sasa wengine wanakuambia tu hawataki kuwaleta. waweke hapa
Nabii Hebron: Huyu walishamuua aisee. sawasawa?! Wameshamuua, wamechukua nyota, walitaka kumtoa kafara.
Nabii Hebron: Baba,… Emmanuel narejesha akili yako sasa ukapate kunielewa, ukapate kunisikia,  hiki kinachokunyonga hapa ninakichomoa.. Jini liko hapa. Sasa haya mafuta hata kama umelishwa kitu gani hakibaki, ninaondoa na tiketi ya mauti. Anakuja Sasa hivi na kichwaa hakuna bwana.
Nakomboa kichwa, majini yaliyoharibu kichwa chake, na mbuzi waliyoichinja na kumzika, ninatupa,… achia haraka.
Emmanuel: (Anakoroma)
Nabii Hebron: Jini hilo.. Piga kelele kwa mara ya mwisho bwana…
Emmanuel: Khanikiiiiiiii…
Nabii Hebron: eee
Emmanuel: Khanikiiiiii……
Nabii Hebron: Wewe muweke chini hapo. Mwache, funika tumbo. Hii ni imani yenye nguvu ndio inatoa hii kitu. Sawa sawa? Sasa
Nabii Hebron: kuambiwa imani leta hela hiyo imeku….
Waumini: imekufa.
Nabii Hebron: Lakini YESU hana makosa, alituma watumishi
Nabii Hebron: Acha kuweka hivi bwana wewe, furahi , unaondoka na mtu wako, mnaenda kula nyama sasa hivi. sawa sawa?
Nabii Hebron: Wakamfanya kichaa..
Nabii Hebron: Sasa huyu, kwa yule anayetaka kuona sasa, kwa somo nililofundisha; Emmanuel, mapepo yaliyokuwa yanakuzuia sasa, mpaka umefika kwa YESU, YESU anamwamsha Emmanuel, amka, Emmanuel amka ukiwa na akili zako, na ukichaa ukiwwa hamna tena.
Nabii Hebron: Eeeeee… Muacheni
Nabii Hebron: Hebu mwacheni bwana.
Nabii Hebron: Leta maiki (mic)
Nabii Hebron: Emmaneul
Nabii Hebron: Emmanuel
Nabii Hebron: Vipi?
Emmanuel: Niko wapi?
Nabii Hebron: Hapa?
Nabii Hebron: Hapa kanisani
Nabii Hebron: Anaangalia hela yake iko wapi au ni nini?
Nabii Hebron: Pesa?
Emmanuel: Pesa na Simu
Nabii Hebron: Nini unatafuta?
Emmanuel: Pesa na Simu
Nabii Hebron: Imeenda wapi?!
Nabii Hebron: Enhe…Imeenda wapi? Umeiona?
Nabii Hebron: enheee… hebu Simu unayo aisee? sasa unaona amerudi na akili!
Ndugu wa Emmanuel: Nimempa mama, mke wake
Nabii Hebron: sasa unaona amerudi na akili, alikuwa hakumbuki hata simu. njoo mama hapa.
Nabii Hebron:Alikuwa na kichaa sasa hamna kichaa tena.
Nabii Hebron: Enhe, vipi mama, unaonaje sasa?
Nabii Hebron: Ukichaa umetoka anachukua mtoto wake
Nabii Hebron: Si alikuwa kichaa sasa hivi?
Nabii Hebron: Emmanuel, Huyu ni mtoto wako?
Nabii Hebron: Ni mtoto wangu huyu.
Nabii Hebron: unamependa?
Emmanuel: Nampenda.
Nabii Hebron: Hebu mbusu.
Nabii Hebron: Na huyu ni mke wako?
Emmanuel: Ni mke wangu
Nabii Hebron: Mke wako?
Nabii Hebron: Unampenda?
Nabii Hebron: Hebu mbusu na yeye
Nabii Hebron: Aisee walitaka kukumaliza. Sawa sawa? Simama hapa, hawakupati tena.
Waumini: Amen
Nabii Hebron: Haya kakae
Nabii Hebron: Anadunda, haya mchukue mtu wako bwana
Nabii Hebron: BWANA YESU ASIFIWE. hiyo ni imani yenye
Waumini: Nguvu
Nabii Hebron: BWANA YESU asifiwe, endelea kuimba, nyoosha mikono
Nabii Hebron: Huyu alikuwa amebakiza masaa matatu afe sasa, mmesikia? Masaa matatu.
Nabii Hebron: Eheee.. mtasema huyu ni kichaa? Mtasema huyu ni kichaa sasa anafuta mtoto wake? eeeh?! ana upendo. Analea baba mzuri.
Nabii Hebron: Hebu muangalie aisee, si unamjua wewe?
Ndugu wa Emmanuel:Leo ni siku ya tatu hajui mtoto wake, mama yake yani hata kuongea alikuwa haongei, hata hanijui mimi niliyekuja naye.
Nabii Hebron: Wewe ni nani wake?
Ndugu wa Emmanuel:Mimi ni mdogo wake
Nabii Hebron: Eeeeeh… aisee anashukuru. Yani anakupa mkono. Mwambie asante
Emmanuel: Asante aisee.
Nabii Hebron: Ulikuwa wapi Emmanuel? Ulikuwa unajua?
Emmanuel: Mimi sijui. sijui.
Nabii Hebron: Tena nikuambie alikuwa amebakisha masaa matatu. Hesabu sasa hivi masaa mangapi bado? Tena kesho abatizwe ili wasimuweze tena.Mmesikia?
Nabii Hebron: Nabii Hebron unamfahamu? wa Arusha?
Emmanuel: Eeeh
Nabii Hebron: Wewe Umetoka wapi?
Ndugu wa Emmanuel & Emmanuel: Kondoa
Nabii Hebron: Umetoka Kondoa?
Nabii Hebron: Kondoa?
Ndugu wa Emmanuel:Yani leo ndio tumetoka huko.
Nabii Hebron: Mlijuaje habari ya hapa?
Ndugu wa Emmanuel:Ndio hivyo MUNGU mkubwa..
Nabii Hebron: Redio?
Nabii Hebron: Au ni mtu amewaelekeza?
Ndugu wa Emmanuel:Tumeelekezwa, na,… na yani yote ni mipango ya MUNGU.
Nabii Hebron: Ilibakiza masaa matatu. Hafi tena.
Waumini: Amen

[ad_2]