Close

MAKANISA 98% ULIMWENGUNI MWOTE YAMEKUWA NI MALANGO YA KUZIMU.

[ad_1]

Ndugu msomaji wa makala ya Mtume Hebron, karibuni tena katika injili ya kweli ya YESU WA NAZARETI aliye hai na sasa yupo mbinguni anasubiri ule mwisho tu aje tena kwa mara ya pili kuwachukua wale walio wake. Ukisoma katika kitabu cha Injili ya Yohana 14:6 “YESU akamwambia, mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa BABA, ila kwa njia ya mimi”. Maana ya njia ndio mlango maana hata kama kuna njia ila mlango umefungwa ina maana hautapita.
Nitaelezea kwa ufupi na naamini utaelewa vizuri maana yeye aliye lango la mbinguni ambaye ndiye YESU ndiye anayenifundisha na zaidi yeye ni mwalimu wa tofauti sijawahi kuona wala kusikia anayefanana na yeye  katika ulimwengu huu, na zaidi hata kuwepo zaidi ya mwalimu kama YESU WA NAZARETI. Watu wengi katika ulimwengu huu hawaendi katika kanisa ambalo ndilo lango la mbinguni bali wengi wanashiriki katika makanisa ambayo ni malango ya kuzimu bila kujua na wengine wanajua. Ila 80% hawajui kuwa wanaabudu katika malango ya kuzimu na 20% wanajua kabisa ukweli wakiwemo na watumishi, wanaojiita kwa majina ya Nabii, Mitume, Wachungaji, Wainjilisti, Waalimu, Maaskofu na Mashemasi.
Kwa ufupi ukisoma katika nyaraka mbali mbali utaona YESU anasema msiwachaji watu pesa yaani watumishi makanisani. Pengine leteni mizigo yenu kwangu nami nitawapumzisha. Sasa nasema makanisa yamekuwa malango ya kuzimu sababu yanayotendeka siyo ya YESU na kama siyo ya YESU ujue hapo tayari YESU hayupo bali ni yesu wa uongo na mahali pa yesu wa uongo ni kuzimu na yeye ndiye njia ya kwenda kuzimu, na ili uingie kuzimu ni lazima uyafuate yake ndio njia yake, na njia yake ni kubadilisha Neno la MUNGU. Mfano wa njia zake za uongo- ukifika kanisani mtumisi ili umuone lazima uchajiwe pesa. Au ukifika kanisani badala ya wewe kuvuliwa mizigo yako uliyonayo ya kiroho, unabebeshwa mizigo na mtumishi ya harambee, michango, na hata kuahidi kiasi cha pesa. Sasa jiulize, je ungemkuta YESU WA KWELI, angekufanyia hayo? Jibu, siyo, sasa elewa hapo ni lango la kuzimu. Watu wengi wamekata tamaa na kanisa sababu ya mambo yanayofanyika kanisani kinyume na Neno la MUNGU. Nawaeleza ni bora mkae nyumbani kuliko kwenda katika lango la kuzimu, unapoendelea kushiriki katika kanisa ambalo linatenda tofauti na biblia, ujue wazi kuwa wewe unaendaga katika lango la kuzimu na siyo lango la mbinguni. Katika lango la mbinguni hakuna mambo hayo.
Nikuulize swali, je wewe unapoenda kanisani unamfuata YESU? Jibu, ndiyo. Sasa kama umemfuata YESU kwa nini uiabudu sanamu? Je YESU ni sanamu? Jibu, siyo. Sasa utabisha wewe haushiriki ibada ambazo ni malango ya kuzimu? Neno la MUNGU linasema usiabudu sanamu, sasa makanisa yanaruhusu kuabudu sanamu, kuibusu, na hata kuwaabudu wanadamu aliowaumba MUNGU. Na wengine hata kuabudu viungo vyao, mfano mioyo yao badala ya kumwabudu MUNGU peke yake maana hata hivyo mnavyoviabudu ni yeye kaviumba. Ni DHAMBI kubwa sana, na ni chukizo kwa MUNGU, bali ni furaha kwa shetani watu kuabudu sanamu ni kumtukuza shetani na wote wanaoabudu sanamu hawamtukuzi MUNGU aliye hai ila wanamtukuza shetani na shetani amekuwa ndio mungu wao na  anawapeleka kuzimu wote, ila elewa na upone leo roho yako.
Jambo lingine lipo wazi kabisa, ili ujue makanisa mengi hayawapeleki watu mbinguni bali yamekuwa ndio njia ya mauti ya milele. Alichokifanya shetani alilibadilisha Neno la MUNGU na ikawa ni kinyume. Mfano ukiona au kusikia mtumishi anakuchaji pesa ndio akupe msaada wa kiroho au kukuombea na kukubariki ndugu msomaji hilo silo Neno La MUNGU wa kweli hata ukisoma katika biblia halipo, na kama unashiriki na wewe umeifuata njia  ya kuzimu either kwa kujua au kutokujua. Sasa uelewe umepewa neno la shetani na hata huyo mtumishi upate picha kabisa kilichojaa ndani ya moyo wake ni maneno ya shetani na ndiye anayemuongoza haijalishi anataja jina la YESU. Yeye alisema watakuja Makristo wa uongo. Mtawatambuaje angalia matendo yao na kuzichunguza roho zifanyazo kazi ndani yao, je ni za YESU WA KWELI au wa uongo. Ukisikia mtumishi anatenda tofauti na biblia ilivyoandikwa ujue tayari huyo mtumishi ni muongo, anasambaza maneno ya lusifa au sumu ya kuangamiza roho za wana wa MUNGU, na zaidi yeye ndani yake ni njia za kuzimu zimejaa na siyo njia ya mbinguni. Japo hata sema anawapeleka kuzimu kimwili ila katika ulimwengu wa roho tayari mmeshakuwa mateka wa shetani. Hii ni sababu ya kufuata njia za maneno ya uongo au kuipindisha Neno la MUNGU
MFANO WA NJIA YA KUZIMU
Ø Mtumishi akiwa ni freemason, mchawi, mwizi wa nyota za waumini na zaidi 80% ya watumishi wote katika ulimwengu wote ni waizi wa nyota za watu na zaidi wanaiba za waumini wao na hata katika mikutani ya injili wanaoifanya au katika vipindi vya Television au Redio. Ukiangalia au kusikiliza tu nyota yako inaibiwa maana wanayo majini ya kufanya kazi hiyo na utashangaa mtumishi ghafla na yeye anakuwa na utajiri wa ghafla usiokuwa na mwanzo na umaarufu, ila hawa siyo watumishi wa YESU wa kweli hawa ndio makristo wa uongo. Hufanya biashara, huchaji riba (kuwa na benki), ubatizo wa maji ya kikombe, huomba pesa kwa njia ya Television hata Redio ya kusapoti huduma zao na unapoitoa hiyo pesa tu, tayari unaibiwa uthamani wa maisha yako na nyota yako, ni lazima wawe na partners.
Sasa YESU ukisoma Neno lake haya yote amekataa, sasa anachokifanya shetani ni kuhakikisha sheria za MUNGU zimevunjwa kwa kubadili yale ambayo ameyapanga MUNGU. Tazama mfano halisi, Adam na Eva pale bustanini Edeni, MUNGU aliwapa Neno lake, msile mti ule wa katikati ya bustani, ila shetani akamdanganya Eva wewe kula, Eva na Adam wakala na walivyokula wakajikuta wapo uchi na kujuta. MUNGU akatamka mume utaishi kwa jasho lako yaani ufanye kazi ngumu na mke utazaa kwa uchungu na ikawa mpaka leo hii ndivyo ilivyo.
Watu wengi wanafikiri  MUNGU hawaoni mnavyobadilisha Neno lake yeye hunyamaza na hata mnavyobadili Neno lake, jicho lake linaona kila kitu. Tazama hata Adam na Eva walifikiri MUNGU hawaoni, walipomaliza kula tunda, akaja MUNGU akawauliza mmefanya nini? Hivyo ndivyo itakavyokuwa kila anayebadilisha biblia na yeye ataulizwa ila tofauti ya nyakati zile na sasa, kipindi hiki MUNGU ameshatoa maelekezo ya kila atakayebadilisha Neno lake (Ufunuo wa Yohana 22: 18-19) ni HUKUMU hata wanaoshiriki ni HUKUMU, toka huko utapona roho yako.
Ø Neno la MUNGU linasema katika Wagalatia 1:6-10, Neno limebadilishwa na kama limebadilishwa ina maana wamemfuata yeye aliyelibadilisha awapeleke huko atakalo yeye kuzimu. Mfano; imeandikwa utoapo sadaka yako asijue mtu, tazama leo hii watu wanaandika majina sadaka zao na wanapewa risiti na rekodi zao zinatunzwa makanisani ambapo ndipo malango ya kuzimu. Mtumishi anayefanya hayo muulize je hili ndilo Neno la MUNGU? Jibu hana, bali hilo ndilo neno la shetani unashirikishwa na wewe neno la shetani umkufuru ROHO MTAKATIFU.
Ø Makanisa yanayoruhusu pombe na hata kuzibariki (Neno linasema usimpe mwenzako kileo) haya ni makanisa yaliyo malango ya kuzimu na yamekubaliana na maneno ya shetani, ndiyo yamekuwa njia yao na ule mwisho shetani atawafungulia mlango waingie kuzimu maana wamekubali kuufuata uongo wake na wamekuwa ni wake.
Ø Makanisa au watumishi wanaofanya biashara haramu wote hao ni malango ya kuzimu, hata kuchangisha pesa kanisani. Tazama YESU aliingia hekaluni akasema nyumba ya BABA yangu ni nyumba ya sala tu ila nyie mmeifanya ni nyumba ya wanyang’anyi, akawatimua, ila leo wanayarejesha. Tayari  ni lango la kuzimu.
Ø Watumishi wote waliojenga makaburi yasiyo na maiti na misalaba, huyo ni mlango wa kuzimu, na wanatabia za KUACT wanalia na pia muelewe huwa wanafanya re-aso za mazoezi ya sauti kabla hajaja kanisani na hujipaka mafuta ya kipepo. Sura zao hung’aa sana na hupenda kujichubua ngozi. Hayo ni masharti na ukimjua mtumishi anayejichubua, mtumishi huyo katika ulimwengu wa roho yeye ni shoga ameolewa na majini. Hivyo yampasa ajirembe kama vile mwanamke kimwili anavyojiremba ili kumfurahisha mmeo. Na wao huwafurahisha majini yaliyowaoa na huwasaidia kufanya kazi za miujiza ya kipepo na kuiba nyota na kuedeleza malango ya kuzimu katika pango hilo (kanisa). Na pia wanazo perfume za kipepo ambazo akijipulizia ni harufu za majini  kila utakayenusa harufu hiyo utaipenda na utamfuata tu (perfume ina majini kivutio), na majini mengine yanakaa katika saa anayoivaa ukiiangalia tu ameshakuteka ufahamu na hata pete za ajabu katika mikono yao na cheni za shingoni (hivi vyote uwe makini wanaweka vyombo vyao vya kuwanasa wana wa MUNGU na kuwapeleka kuzimu). Na ili akuteke ni lazima akukamate ufahamu wako, ila YESU amenituma niwafungue hata fahamu zenu muwe huru. Sasa hivi kanisa linanuka harufu mbaya mbele za MUNGU, na kama linanuka ina maana MUNGU amelipa kisogo. Utakavyo soma ujumbe huu, watumie na wenzako wasome, utakuwa umemfurahisha YESU WA NAZARETI, maana wengi watapona na shetani kuaibika.
Ø Mtumishi aliyopo kuzimu lazima awe lango la kuzimu na yeye ukiona anagawa stika ndizo zenye nguvu ujue hiyo ni hirizi na unapokuwa nayo tu maisha yako yote ni Baraka zako anazichukua yeye. Kwa kifupi kila mtumishi anayeuza stika halafu anakueleza itakulinda huyo ni MCHAWI na hiyo stika ni MAJINI, na yeye ni lango la kuzimu la kristo wa uongo.
Ø Na inawezekana mtumishi mwanzoni alikuwa anatumika na MUNGU ila akaacha njia zake na MUNGU humwacha. Mfano ukikuta kanisa linamuabudu Nabii, Mtume, Mchungaji kama yeye ndiye MUNGU ujue tayari yeye ndiye lango la kuzimu. Imeandikwa utukufu wangu sishirikiani na mtu au chochote, sasa ona hapo tayari amevunja amri ya Neno la MUNGU. Au anabatiza kwa jina lake huyo tayari ni mpingaji wa Neno la MUNGU na siyo mtenda Neno bali ni mvunja Neno la MUNGU. Hata kama anasema analishika neno, je huko ndiko kulishika neno na kulitenda? Jibu, siyo. Pakishakuwa tofauti na Neno la MUNGU hapo tayari ni lango la kuzimu, maana pangekuwa lango la mbinguni pangelitii Neno la MUNGU na kulitende. (Kumbukumbu La Torati 6: 1-25).
Ø Makanisa yote yanayofungisha ndoa za jinsia moja hayo yote ni malango ya kuzimu (1 Timotheo 1:8-10).
Ø Makanisa yote yenye BAR, CLUB.
Ø Makanisa yote yenye BENKI.
Ø Yenye masanamu ya aina yeyote (Kumbukumbu La Torati 4: 15-23), lakini hili Neno la MUNGU limebadilishwa na kuwekwa la shetani ambalo halipo katika kitabu cha Neno la MUNGU.
NOTE:
Ndugu msomaji ninakupa shule fupi uelewe japo kiasi na mengine ROHO MTAKATIFU akufundishe ili upone roho yako usidanganyike ukafikiri unaenda katika lango la mbinguni kumbe unapelekwa au upo katika lango la kuzimu bila kujua. Sasa upone roho yako, sasa hivi mambo yameharibika na shetani anajua Anytime JESUS is coming back for the second time, anachokifanya ni kutengeneza malango yake katika makanisa na kubadili Neno la MUNGU, na makanisa yote yaliyobadili neno au kutenda tofauti na Neno la MUNGU hiyo ni picha halisi kabisa tayari hapo siyo lango la mbinguni tena ni lango la kuzimu.
Hata kanisa ambalo linafufua misukule hilo ni lango la kuzimu hayo ni mazingaumbwe full, ili ujue ni wachawi na siyo nguvu za YESU wa kweli, waambie waende mochuari kuna maiti nyingi, watakimbia hao watumishi. Hiyo ni njia rahisi kuwajua makristo wa uongo na wapo kuzimu na hapa ulimwenguni kazi zao ni kuimarisha ufalme wa shetani na malango yake. Hivyo ukristo wa kweli imebakia 2% katika ulimwengu wote. 98% yote ni ya uongo. Chunguza Neno la MUNGU kanisa kwa kanisa na mtumishi kwa mtumishi, utapata jibu. Mike zao ndani zina nyoka, akiongea au kukuhubiria anamwaga makufuru tupu. Hata kubarikia watu wazima tayari ni kubadili Neno la MUNGU na kufanya maneno ya shetani.
Soma vitabu vya Nabii Hebron utafunguka. Elimu hii ni YESU ndiye kanifundisha aliponiita nikamtumikie akaniambia Hebron nimesalitiwa na watumishi sasa nenda uifanye kazi yangu. Wakimsaliti YESU ndiko kufanya ya shetani na kujenga malango ya kuzimu ndani ya kanisa.
NABII HEBRON.

[ad_2]