MAMILIONI YA WATU KATIKA ULIMWENGU HUU WANAZO SHAHADA ZA VYEO VYA SHETANI

[ad_1]


Hili silo jambo geni katika ulimwengu huu ambao MUNGU alituma mwanae wa pekee YESU WA NAZARETI aje aukomboe ulimwengu huu na watu wote kwa njia ya Toba na kumwamini yeye na kuokoka, hakuna njia nyingine ya kufanya mtu yeyote apone roho yake isipokuwa ni kuokoka peke yake au njia ya kwenda mbinguni na njia hii ndiye YESU, ambaye yeye ili akupeleke mbinguni lazima uwe na vyeo vya mbinguni yaani utakatifu, wokovu na matendo mema na kulishika Neno lake na siyo kulibadilisha.
Shahada hizi za shetani zipo shahada mbali mbali kwa majina yake sawa sawa na cheo chake, vyeo vikubwa vya shetani walivyonavyo na wamevipokea na kuvikubali ya kuwa wao ni watendaji wa shetani ni dhambi. Vipo vyeo vya aina mbali mbali vya shetani:
1.      Vyeo vya mpinga kristo.
2.     Kila mchawi, mganga wa kienyeji, mnajimu,wapiga bao (ramli) hawa wote wana vyeo vya shetani na hizo kazi wanazozifanya ndizo shahada walizopewa kutoka chuo kikuu cha shetani ambacho makao yake yako kuzimu.
3.      Watumishi freemason wote.
4.     Watu wote wanaofufua misukule
5.     Ulevi, uzinzi, uongo, rushwa, chuki, wivu, kuabudu sanamu, hata mitume waliopita, ushirikina, uwizi, ufisadi.
6.     Kutambika (matambiko).
7.     Ubatizo wa maji ya kikombe.
8.     Kubatizwa kwa jina la mchungaji.
9.     Kubusu picha za aliye ACT filamu ya YESU.
10.                       Kuongozwa na majini na mapepo
11.                       Wezi wa nyota
12.                       Watumishi wanaotumia uchawi au waliojiita hawajulikani na MUNGU.
NOTE:
Watumishi wote wanaozini na waumini au wake za waumini hao wote ni watumishi wenye vyeo vya shetani siyo vyeo vya YESU, na kama wana vyeo vya shetani basi baba yao ni shetani. Usidanganyike muwe makini, hakuna watu wachawi kiwango cha kutisha kama wanaojiita Manabii, Mitume, Wachungaji, Wainjilisti, Waalimu.  Wameshinda hata waganga wa kienyeji, japo hata wachawi na wao wanajua watumishi wamewashinda kwa nguvu za uchawi. Muangalieni YESU WA NAZARETI, hata linalojiita kanisa kwa jina lake sasa hivi 98% katika ulimwengu wote linaongozwa na watumishi   waliomsaliti YESU. Chunguza matendo yao, kila mtu hata mchungaji wako mchunguze matendo yake, jibu utalipata, hayo matendo maovu ndiyo vyeo vya shetani na katika kanisa analoliongoza anawamwagia waumini hivyo vyeo vya shetani kwa njia ya kinywa chake. Ndiyo maana makanisani watu ni walevi, wazinzi, hii ni sababu ya kuhani ni mchafu anayo vyeo vya shetani.
ØSwali, je wewe unacho cheo cha shetani? Jibu, unalo.
ØJe hiyo michanganyo ya dhambi (vyeo vya shetani) wewe  umeajiriwa na shetani? Sasa kwa nini unatenda dhambi? Ina maana amekuajiri yeye na umemtii ndiyo maana  unamtii tajiri yako.
ØWacha kuwa mwajiri wa shetani, mrejee MUNGU akupe vyeo vyake ambayo ni utakatifu.
NOTE:
Kuabudu sanamu na wanaoabudu sanamu ni watenda kazi wa shetani na bila kuacha hautaenda mbinguni, kifupi hao ni wapinga kristo full, kama ulikuwa haujui sasa elewa, YESU siyo sanamu, ni mwana wa MUNGU aliye hai na yupo mbinguni, ila mapepo ndiyo yapo kwenye masanamu. Zaidi endelea  kusoma makala na pia karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOZI WA MATAIFA YOTE, utafundishwa mengi kuhusu YESU WA NAZARETI na utakutana na yeye maana yupo na ni yeye ndiye aliyelijenga na milango ya kuzimu hailiwezi milele na litaenda ulimwengu wote na MUNGU ndiye kiongozi atakaye ongoza injili yake na kuung’oa ufalme wa shetani na wafanyakazi wake na serikali ya shetani kuangamia. Na tayari kazi  hii ameshaianza YESU peke yake, aliye YESU WA NAZARETI wala siyo yule yesu kristu wa uongo (kristo wa uongo).

NABII HEBRON.

[ad_2]