MARTIN LUTHER NI MMOJA WAPO WA WATUMISHI WANATESEKA WALIOPO KUZIMU!!!

[ad_1]

Ujumbe huu ambao nawaeleza ni YESU WA NAZARETI ndiye aliyenionyesha na mimi nikawaona kwa macho yangu, japo inatisha ila nitawaelezea kwa kifupi na sababu ya mimi kuonyeshwa ni ili niwaeleze ulimwengu wote wajirekebishe na wamrejee YESU WA KWELI na siyo wa uongo na kuzifuatia hadithi za uongo na elimu ya uongo katika makanisa yote. SOMA 2 Timotheo 4: 1-4.
Mnamo 2013 BWANA YESU alinichukua akanionyesha picha ya kuzimu jinsi ilivyo halisi na waliopo huko ambao wanasubiri hukumu na mlango wao kwenda mbinguni umeshafungwa. Niliona ofisi za kuzimu na serikali zake, kwa vitengo mbali mbali, ila nitaelezea kwa kitengo cha kanisa cha kuzimu. Ipo wizara ya kanisa la kuzimu na ndiyo inayowapa watumishi wa kipepo nguvu za miujiza ya shetani na kuwapa vyeo kwa kufananisha na huduma tano za kanisa. Shetani amecopy kila kitu na yeye akawaita wa kwake wachungaji, manabii, mitume, waalimu, wainjilisti. Ila wewe kwa macho yako ya nyama ya kibinadamu hauwezi kuwajua maana hata mimi Hebron sikuweza kuwajua miaka yote mpaka aliponifundisha YESU mwenyewe, maana mimi kazi yake ananifundisha yeye peke yake, na wala sijaenda chuo chochote cha kibinadamu katika ulimwengu huu.
Ilipofika wakati wa kunionyesha watumishi waliopo kuzimu niliona ni mamilioni ya watu, nikamuuliza YESU hawa si watumishi wako mbona wapo huku badala ya paradiso. Akaniambia, mwanangu Hebron nimeamua nikuonyeshe uyaone na wewe, nilikuisha kueleza katika siku za mwanzo 2010 nilipokutana na wewe tukiwa wawili tu, nilikuambia nataka mwili wako tu nipeleke injili yangu mimi peke yangu nitaishi ndani yako. Hao niliowatuma wamenisaliti mimi wameamua kumfuata shetani, ila hapa ulimwenguni kimwili hunitaja kwa midomo yao ila ndani ya mioyo yao ni mbwa mwitu. Mimi niliwaita watumishi wachache tu na siyo wengi kama inavyoonekana katika ulimwengu huu. Wengi wamejiita, wanajifanya, wanatafuta pesa, wengine ni wa kanisa la kuzimu. 98% ya watumishi wote ulimwengu huu siyo watumishi wangu mimi YESU WA NAZARETI ni watumishi wa kristo wa uongo.
Akanionyesha mmoja wa waanzilishi wa dini katika ulimwengu huu na alikuwa amefungwa mnyororo mkubwa katika kiuno kwenye mhimili wa chuma, nikamuangalia kwenye paji la uso wake nikaona jina lake Martin Luther, nikashtuka maana mimi kwa akili zangu nilijua atakuwa paradiso. Akaniambia, usiogope, nikamuuliza YESU huyu anafanya nini huku na ni mtumishi wako, akaniambia, Hebron huyu sijamuita anitumikie na wala hata katika kitabu cha listi ya watumishi waliotoka kwangu huyu hayupo, wala sijamtuma. Niliogopa zaidi, akaniambia huyu amefanyika kuwa geti la kuwazuia watoto wangu wasije mbinguni akianzisha dini yake ambayo mimi sijamtuma na kama sijamtuma ujue yupo aliyemtuma, akampa maneno yake na uwezo wa kufanikisha kusudi hilo. Akaniambia, Martin Luther ningekuwa ni mimi nimemtuma angelitenda Neno langu. Akaniambia, Hebron, ubatizo wa maji ya kikombe umetoka kwa MUNGU? Nikajibu hapana, akaniambia hilo ni moja uelewe, alichokianzisha siyo Neno langu, pili mimi nilionyesha njia nikiwa mtoto mdogo nilibarikiwa tu na nilipokuwa mtu mzima ndiyo nilibatizwa, ila yeye ametenda kinyume na ubatizo wangu. Akaniambia, mimi sijaruhusu sadaka ya ahadi na collect, akanimabia sadaka ya ahadi ni agano kati ya mtu na Martin Luther ya kuwa wewe ni wa Martin Luther na mtu siyo wa kwangu.
Akaniambia hivi watu wanatakiwa waitwe kwa jina langu au kwa jina la mtumishi? Nikamjibu wanatakiwa waitwe wakristo, sasa kwa nini hawa wanajiita ni wakristo halafu wanajiita kwa dhehebu la aliyelianzisha? Akaniambia ukijiita kwa jina la aliyeanzisha dhehebu ina maana wewe ni wake na mimi YESU sikupati wewe na hata ule mwisho nikija nitakuja kuwachukua wale waliookoka na ni watakatifu tu ndiyo nitakaowachukua, ila kila aliye kinyume uwaeleze watu wote na kwa mataifa yote sitamchukua mimi YESU sipo kinyume na BABA yangu letu ni moja. Waeleze mimi sijaanzisha madhehebu wala dini. Dini na madhehebu yalikuwepo hata kabla yangu mimi YESU kuja kimwili ulimwenguni. Na kazi ya dini siku zote ni kubadilisha Neno la MUNGU na kuweka uongo ndani yake, kama ilivyo ubatizo wa uongo, ubarikio wa uongo, hayo yote ni maneno ya shetani yaliyoingizwa katika makanisa ili kuwapiga watu upofu wapotee kama ilivyo sasa.
Nimekufunulia siri hii na wewe uwaeleze watu wote na mimi ninaangalia kila anayeusoma ujumbe au kuusikia asipotii haya ajue na yeye ataungana na Martin Luther katika mateso milele. Akasema kwa hasira kweli, OLE wao na hao waliopo hai katika ulimwengu wanaobadilisha Neno langu na kusimamisha mizizi ya shetani ndani ya mioyo yao, waeleze na wao mahali pao ni kuzimu. Ila wapo ambao hawajui Neno langu na wengine wanajua kabisa wanafanya makusudi. Waeleze wanirejee mimi wafuate njia zangu, kinyume na hapo Jehanamu inawahusu. Nikamuuliza mbona Martin anajulikana ni mtu maarufu katika ulimwengu? Akaniambia, kwa MUNGU ni haki peke yake na utakatifu, ghafla akanionyesha watu maarufu waliokufa wakiwemo maraisi, wafalme mbali mbali akiwemo Herode, matajiri maarufu, akaniambia angalia na hao wapo wapi? Akanimabia hawakuwa watakatifu na hawakuokoka. Akaniambia pando ambalo mimi sikulipanda nitaling’oa na kulichoma moto liteketee, mafundisho ambayo hayajatoka kwangu na kila aliyeanzisha watu wakayafuata hao wote mahali pao ni jehanamu, na wote wanaoendeleza mafundisho ya uongo watajumuika nao hapa hapa kuzimu. Akaniambia, ujumbe wangu uufikishe tena haraka, nikasema ndiyo BABA, nami nawaeleza watu wote jamani okokeni kikweli, kuzimu kuna mateso yasiyoelezeka na Malaika Gabriel yupo makini kuchukua roho itokayo kwa mtu wakati wa kufa anaipeleka kwenye matendo yake, kama ni matendo ya giza ni kuzimu unasubiri jehanamu, kama ni mtakatifu utakaa paradiso ukisubiri ule mwisho ila hauteseki unakula raha.
Akanimabia, waeleze mtu anapokata roho tu ndiyo mwisho wake anapelekwa kule alichokipanda ndicho atakachovuna. Ila watu wameletewa mafundisho ya uongo wakifa wataombewa ili wapokelewe, akanieleza, waeleze hao wote ni waongo ndani yao ipo roho ya mpinga kristo ili kuwazubaisha watu wasinijue mimi YESU na wasifike nilipo mimi. Waeleze mataifa yote wanirejee, muda wangu umekaribia kurudi kwa mara ya pili, ila watu wengi ni wa shetani. Makao nimeshayatengeneza kama nilivyoahidi naenda kuwatengenezea makao, ila haya makao hayana watu wa kukaa, waeleze watakaokuja kwenye makao niliyoyaandaa ni wale walio wangu tu. WAMEOKOKA NA WATAKATIFU 100%. Wengi watalia na kusaga meno maana nitawaambia sikujui sikujui, sababu ya matendo yao. Na zaidi YESU akaniambia madhehebu na dini siyo matawi yake ni matawi ya shetani na kila tawi ambalo silo lake yeye hulikataa. Akaniambia ndiyo maana Martin Luther yupo huku kuzimu sababu siyo tawi langu, niliogopa zaidi maana sikuyaelewa haya, waeleze atakayesikia atapona atakayepinga na yeye ule mwisho wake ataungana nao na kufungwa minyororo kuzimu.
SALA YA TOBA:
YESU WA NAZARETI NAOMBA UNISAMEHE UNIANDIKE KATIKA KITABU CHAKO CHA UZIMA WA MILELE, UNIONGOZE MILELE NISIPOTEE, AMEN.

NABII HEBRON. 

[ad_2]