Close

MJUE YESU KRISTO WA KWELI NA YESU KRISTO WA UONGO

[ad_1]

MJUE YESU KRISTO WA KWELI NA YESU KRISTO WA UONGO

Ndugu msomaji na mwanadam yeyote wa taifa lolote kwa rangi yoyote na jinsia yoyote na kwa umri wowote na hata viumbe vyote, milima, wanyama wa nchi kavu na majini, mwezi, nyota, na kwa ujumla vitu vyote pamoja na ulimwengu wote na sayari zote. Hivi vyote ni mali ya MUNGU aliye hai ambaye ndiye BABA yake YESU KRISTO wa Nazareti / au kwa jina lingine YESU wa Galilaya na mwana pekee wa MUNGU;  nakusalimu kwa jina la YESU KRISTO wa Nazareti, au watu wengine wanamwita Nabii Issa ili uelewa vizuri.
Ndugu msomaji, siku ya leo imempendeza MUNGU kuwafungua ufahamu na kumjua YESU KRISTO wa Nazareti, aliye YESU wa kweli, na pia kumjua Yesu Kristo wa uongo, ili msipotezwe tena na mpone. Soma katika kitabu cha injili ya Mathayo 24:23-25; NENO la MUNGU linasema, wakati huo mtu akiwaambia tazama KRISTO yuko hapa au yuko kule msisadiki, kwa maana watatokea Makristo wa uongo na Manabii wa uongo, nao watatoa ishara kubwa na maajabu; wapate kuwapoteza kama yamkini hata walio wateule. Tazama nimekwisha waonya mbele.
Ndugu msomaji, nafikiri watu wengine mnasikia nasema kuwa yesu kristo wa uongo, unanishangaa; sawa, na ninaposema kuwa YESU wa kweli unanishangaa, usiogope, leo utafunguka 100%. Kwanza kabisa nitakueleza maana ya YESU, au YESU ni nini? YESU maana yake ni MUNGU pamoja na sisi, tunajua kuwa miungu mingi hapa ulimwenguni zaidi ya huyu MUNGU aliyeuumba ulimwengu huu. Mfano, shetani ni aina ya mungu pia. Hebu jiulize, sasa katika injili ya Mathayo 24:24 (a)Kwa maana watatokea Makristo wa uongo, sasa nikuulize wewe ndugu msomaji, tazama hata Biblia imeandika. Na zaidi, soma katika kitabu hiki cha injili ya Mathayo 24:4-5,11. YESU huyu wa Galilaya na Nazareti, nanukuu kama Biblia inavyosema, YESU akajibu akawaambia, angalieni, mtu asiwadanganye. Kwa sababu wengi watakuja kwa jina langu, wakisema mimi ni Kristo; nao watawadanganya wengi, mstari (11) na manabii wengi wa uongo watatokea na kudanganya wengi.
Ndugu msomaji, YESU alikwishasema angalieni mtu asiwadanganye ila kwa sasa yametimia 98% na ulimwengu unaongozwa na huyu yesu wa uongo, na ambaye YESU huyu wa Nazareti aliyajua hayo yatatokea, na watatumia jina lake kwa ajili ya kuwapoteza hata wewe mteule ili uangamie, ila sasa haya yamefichuliwa na MUNGU, na nitakufunisha vizuri ili roho yako ipone. Kwanza kabisa nitakueleza ufunuo huu wa kumjua yesu kristo wa uongo ambao pia YESU wa Nazareti ambaye ndiye YESU wa kweli na mwana wa MUNGU wa pekee, alishatabiri au kuyasema ni ya  kweli 100%, ila wanadamu walipigwa upofu na kushindwa kutofautisha YESU wa ukweli ni yupi na wa uongo ni yupi na yukoje. Nitakueleza kwa ufupi tu, ila masomo mengine utayapata katika vitabu nilivyoandika, na CD, DVD na Tape.
Joka kuu ambaye ndiye baba yake shetani alivyofukuzwa mbinguni, alipofika kuzimu, joka huyu alitengeneza serikali yake kwa kuiga mfano wa pich ya Mbinguni, nitaeleza kwa kifupi, ila endelea kufuatilia masomo na vipindi nya Nabii Hebron. Nitaendelea kuelezea kwa jinsi ambavyo ninayoelezwa niwafundishe, nsidanganyike kama mnavyodanganyika 98% ulimwengu mzima, wala mimi sipunguzi neno, wala kuongeza lolote, nampenda YESU wa Nazareti. Huyu joka kuu ndiye aliyemzaa yesu kristo wa uongo, na huyu yesu kristo wa uongo ni aina ya malaika wa shetani (na ndiye yesu kristo wa uongo).
Ndugu msomaji, jiulize kwa nini YESU alisema makristo wa uoongo watawadanganya wengi, YESU wa Nazareti, anayo maana kuwa, kristo huyo wa uongo, baba yake ni baba wa uongo. Baba wa uongo ni shetani. Natumaini unazidi kufunuka ufahamu wako (soma Mathayo 24:5). Yesu huyu wa uongo makao yake yalikuwepo kuzimu, ila kwa sasa hayapo tena, mimi Hebron kwa kuongozwa na YESU KRISTO wa Nazareti alinifunulia siri hii, na kuniamuru nimkamate na kubomoa serikali yake yote. Nilimaliza kazi hiyo tarehe 2 Machi 2013 majira ya saa kumi na mbili jioni kwa masaa ya Afrika Mashariki (Tanzania).
Huyu yesu wa uongo alikuwa ndiye mwanakondoo wa joka kuu kwa ajili ya kuuangamiza ulimwengu wote. Yesu huyu wa kuzimu alijitengenezea majina ya watakatifu wa mbinguni, akawaita wengine hivyo hivyo, akiwamo Yuda Iskarioti. Huyo hata mbinguni hayupo. Wakawa wanalo kanisa kubwa sana ambalo yesu wa uwongo ndiye analiongoza, na lilikuwa na nguvu sana, na nuvu hizo zilikuwa wanapewa  watumishi waliopo ulimwenguni humu ambao wamemsaliti YESU au kwenda kinyume na MUNGU wa Ibrahimu alivyopanga. Na siri hiyo wale watumishi waasisi wa baadhi ya dini ulimwenguni hapa wanajua kabisa ila sasa mwisho umeshafika, mtayaona. Kazi ya huyu yesu wa kuzimu ni kubadilisha mpango wa MUNGU aliye hai na kuweka mpango wake wa mungu mfu ili wanadamu ile siku ya mwisho waende kwa mungu mfu, na hata kwa sasa 98% ya vifo vya Wakristo wanaokufa, hawaendi kwa YESU wa Nazareti, wanaenda kwa yesu wa kuzimu. Yesu huyu wa kuzimu anacho mpaka kitabu cha uzima wake wa kuzimu, kama ilivyo, tunavyojua mbinguni YESU KRISTO wa Nazareti anacho kitabu cha uzima wa milele. Huu ni ujanja wa shetani sababu binadamu wanampenda YESU wakisikia jina lake, ila hawamjui ni wa Galilaya au ni wa kuzimu. Leo utafunguka, ila wengi watumishi mnaoupata ujumbe huu mnajijua nyie mnawaangamiza watoto wa MUNGU; nawatangazia baba yenu wa uongo hayupo tena na gadhabu ya YESU KRISTO wa Nazareti ipo kazini. Ndugu msomaji, hivi haushangai imeandikwa siku ya mwisho wengine watajitetea, BWANA, kwa jina lako niliponya, kwa jina lako nilitoa mapepo, na BWANA atasema sikujui, mahali pako ni kwenye lile ziwa la moto. Funguka ufahamu, kwa nini mtu atumie jina la YESU kuponya halafu akataliwe siku ya mwisho? Ina maana hakuongozwa na YESU wa Nazareti au wa Galilaya. Aliongozwa na YESU wa uongo na huyo huitwa nabii wa uongo maana baba yake ni yesu wa uongo. Huyu yesu wa uongo amejenga makanisa mengi ulimwenguni 98% ni makanisa yake, na humo jina la YESU linatajwa kawaida, na Biblia husomwa. Kwa kubadilisha yale ya MUNGU wa kweli yasifuatwe ili kukupata wewe kama wengine 98% walivyopatwa. Hebu jichunguze.
Nitaelezea kwa kifupi mifano ya Manabii wa MUNGU waliopita ambao wapo mbinguni kwa sasa.  Mfano Musa alipokwenda mlimani kuongea na MUNGU, na mara nyingine alipelekwa mbinguni hali akiwa hapa ulimwenguni. Aliamriwa ayafanye yale ambayo ameyaona mbinguni kwa YESU wa Nazareti. Mfano mwingine Yohana mbatizaji aliagizwa aje ulimwenguni abatize kwa maji mengi, haya ndiyo ya YESU wa kweli wa Nazareti. Huyu yesu wa kuzimu au wa uongo ndie muasisi wa ubatizo wa kikombe na wote mliobatizwa ubatizo wa kikombe hamjabatizwa na YESU wa Nazareti, haijalishi limetajwa jina lake, nina hilo ni la kristo wa uongo, na wewe unakuwa mkristo wa uongo! Hata wanaobatiza ubatizo huo wanaongozwa na yesu wa kuzimu. Kama mlikuwa hamjui mfunguke; angalieni kukimbia kwenu na kufanya hiyo kazi isiwe ni bure. Na mwisho ni kilio ukifikiri unamtumikia YESU wa Nazareti kumbe ni yesu wa kuzimu. Ukiangalia kwenye mtandao wa freemason, tafuta majina ya watumishi, jina utakaloliona, ujue mtumishi huyo anaongozwa na yesu wa uongo au wa kuzimu. Usitishwe na jina analolitaja, hao ni wauaji wa watoto wa MUNGU. Zile sala za toba wanazoongoza watu, majina yao huandikwa kwenye kitabu cha uzima wa yesu wa uongo kuzimu. Huyu yesu wa kuzimu hukaa ndani ya dini na watumishi wa makanisa na hutaja jina la YESU ila ndani yao ni roho ya uharibifu juu ya maisha yako, na hata kama ni mtumishi unaependa kurejea kwa YESU wa Nazareti, tubu ili upone, kinyue chake utaangamia japo YESU wa Nazareti ameniambia kuna baadhi yao hata toba yao haitasikilizwa, hukumu ipo juu yao tayari. Ndugu msomaji, natumaini unazidi kufunguka ufahamu wako, na kuanzia leo amua moyoni mwako, na usikae katika madhabahu za yesu wa kuzimu (uongo).
KAZI ZA YESU WA UONGO

Ni kuhakikisha waumini ambao wanayakiri au kuyatenda yale ambayo MUNGU amesema yafuatwe hayafuatwi.
Mfano:

1. Imeandikwa, utoapo sadaka, hata kulia na kushoto isijue. Ina maana asijue mtu. Yesu wa kuzimu alichokifanya kwa kanisa lake unaambiwa andika jina lako, kiasi, namba za simu, na kupewa risiti ya malipo ya sadaka yako. Hivyo ujue sadaka yako imeenda kuzimu na zaidi hata usipoandika jina kwenye sadaka hiyo, na unaitoa katika madhabahu hiyo, bado haipokelewi na YESU wa Nazareti, sadaka bado zimaenda huko.
2.   Haijalishi umeinenea nini, ujue hayo yote yanaenda kwa yesu wa uongo hata ukimtaja YESU wa Nazareti unajisumbua.
3. YESU wa Nazareti hawezi kuja kwenye ngome ya yesu wa uongo wala kukaa hapo, wala hatakaa aje milele. Matokeo yake hauoni baraka, unazidi filisika, unabakia kusoma imeandikwa katika Malaki 3:10,11. Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye wala hataharibu mazao ya ardhi yenu, wala mzabibu wenu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema BWANA wa majeshi. Ndugu msomaji, badala ya wewe kubarikiwa kama NENO la YESU wa Nazareti, imekuwa ni kinyume, unashangaa unatoa sana, sio ajabu hata viti vya madhabahuni umemtolea wewe lakini unapokea baraka za yesu wa kuzimu (kufilisika, hauna mwelekeo, na unapoona hayo tambua kuwa hata safari yako kwenda mbinguni siyo. Unaelekea kwa yesu wa kuzimu maana hayo ndiyo yake.
4.   Kila mtu anajua amri kumi za MUNGU, na mojawapo inasema  usiabudu sanamu, miungu au kitu chochote zaidi ya MUNGU, au hata alichokiumba kwa mfano wake. Lakini siku hizi makanisa baadhi ulimwenguni huku, yanaabudu watoto wa MUNGU, sanamu. Na watu wengi mmeshindwa kuelewa je, si YESU, mbona anatajwa kanisani kwetu? Ni sawa kabisa, YESU wa kweli na wa Nazareti ni mtoto wa MUNGU aliyeandika amri hizo na yeye hashiriki uongo wa kuabudu sanamu au kuvunja amri za BABA yake, mahali hapo ujue ni kanisa la yesu wa uongo ambao YESU wa Nazareti alisema watatumia jina lake kuwapoteza wengi, kama ilivyo sasa wengi wamepotea kwa kudanganywa na jina la YESU wa uongo. Na hao wote watapelekwa kwa baba yao wa uongo, na hapo watu watalia na kusaga meno! Usishiriki ibada hizo, ni bora ukae nyumbani ili usiangamie, ukiendelea kumuomba YESU wa Nazareti akuongoze katika madhabahu ya YESU wa Nazareti. Pia uwe makini unaweza kuta jina la kanisa limeandikwa maneno mazuri mfano: Kanisa la Yesu wa Galilaya, Nazareti, Kanisa la Mungu au la Ufufuo, au jina lolote, ila ukiingia ukikuta watu wapo kinyme na Biblia au ni michango tu, ujue hapo wanaongozwa yesu wa uongo, na wewe unazidi kupigiliwa misumari, hauende popote.
5. Imeandikwa nyumba ya baba yake YESU wa Nazareti ni nyumba ya ibada na sala tu! Kila mtu anajua hivyo, enzi zile YESU wa Nazareti alipokuwa hapa ulimwenguni aliingia hekaluni akakuta wanafanya biashara, YESU huyo wa ukweli wa Nazareti aliingia akatimua kila biashara bila kuogopa (Marko 11:15-18) usome. Sasa mambo haya yaliingizwa na yesu wa uongo katika kanisa, ila YESU wa Nazareti aliyakataa, hebu ona leo hii yalivyo makanisani. Je nikuulize swali, hapo YESU wa ukweli wa Nazareti yupo? Jibu ni yesu wa kuzimu ndio madhabahu yake, Mfano kanisa hilo wanaomtaja yesu wao wanafanya biashara (wana benki). Wkati  YESU wa kweli mwana wa MUNGU alishakataa, na kama amekataa na hilo kanisa linafanya hayo, ndugu msomaji, funguka ujue hapo ni yesu wa uongo na wanatumia jina lake, usishiriki tna, utalaaniwa na MUNGU. Haya ni ya yesu huyu ambaye ndiye kristo wa uongo, maana kazi ya YESU wa Nazareti ni kuhubiri injili ya kweli na ni bure tu.
6.    Imeandikwa nimekupa bure huduma nawe utoe bure. Huyo ni YESU wa nazareti asema hivyo. Utashangaa katika kanisa jina la YESU linatajwa, na unaambiwa toa pesa ndio ufunguliwe. Jamani fungukeni, hyo ni  yesu wa kuzimu (uongo). Na kawaida, fomula ya shetani hatoi kitu bure, lazima utoe kwanza, kwa mfano, unapo /  ulipoenda kwa mganga ambaye pia na huyu ni mtumishi wa shetani 100%, huduma lazima atakuambia toa kitu mfano Pesa, kuku, mbuzi na zaidi hata kuzini na wewe. Ukiyakuta haya, nakuambia kama nilivyoambiwa na YESU wa Nazareti hapo ni YESU wa uongo ndiye anayesimamia, na hamfunguliwi, na hata ukifunguliwa ni kwa muda tu, na hali yako mbaya hurudia mara mia mpaka unajuta ni kwa nini uliokoka badala ya kwenda kuokoka uwe hai, unakuwa umejipeleka kufa, na ndio unakuwa hauna mbele wala nyuma, na mambo hayaendi.
7.   Ukikuta kiongozi wa kanisa ni mzinzi, mlevi au mchawi, wazee wa kanisa wako hivyo, ndugu msomaji, ujue hapo wanaongozwa na yesu wa uongo au yesu wa kuzimu. Haijalishi wananena kwa lugha, hizo lugha sizo za kutoka kwa YESU wa Nazareti. Hata huyo yesu wa kuzimu anakopi lugha hizo, ila zake hazina udhihirisho, na anaponena watu hawaelewi, mnaunganishwa mfe kiroho, na ukifa kiroho, mbinguni kwa YESU wa Nazareti hauendi. Ukikuta mtumishi wa kanisa anazini na hata zaidi kuzaa nje ya ndoa, na hata hatengwi kanisani anaendelea kuhubiri, ndugu msomaji funguka, huyo hana YESU wa Nazareti, huyo ni mtumishi anayeongozwa na YESU wa uongo. YESU wa kweli hakai ndani ya mtumishi mzinzi, madhara yake wote mnarithishwa roho ya uzinzi na laana kwa kanisa hilo lote. Hiyo ni namna ya yesu wa uongo anavyofanya ili mlaaniwe na muangamie, haijalishi ni kanisa la kiroho, hilo ni kanisa la yesu wa kuzimu.
8. Habari nyingine. Ukikuta mahali wanachoma udi halafu wanataja jina la YESU, ndugu msomaji funguka, hapo ni mahali pa yesu wa uongo. Kazi ya udi ule moshi na harufu yake ni chakula cha majini (mapepo). Na udi unapochomwa, yale maroho ya yesu wa kuzimu huja kuongoza ibada hiyo, na yesu wa uongo utasikia anatajwa tu. Wengi mnaonaga sehemu mbalimbali kwenye maduka, hoteli, magari na nyumba yoyote wanayoabudia, ukiona hayo funguka, hapo hizo kazi zao zinaongozwa na majini au sheetani, sasa funguka, huo ni usanii kwa kupitia YESU wa uongo. Udi ni chakula cha majini, hata wengi wenu mnajua, je YESU wa Nazareti anashirikiana na majini? Jibu hapana.
9. Wanaojiita wakristo na wanatumia udi kwenye maisha yao, hao wote hawana YESU wa ukweli, wanaongozwa na yesu wa kuzimu. Hata ibada wanazokwenda ni kujiunganisha zaidi na huyo yesu wa kuzimu, ukiwa mlevi, umezika Biblia kanisani au mahali popote, huyo sio wa YESU wa ukweli, ni wa yesu wa kuzimu  na akikuongoza na wewe anakupeleka huko.
10.  Tunajua ya kwamba nyumba ya ibada ni nyumba ya sala tu, haitakiwa kufanyika kitu mfano kumzika mtu kanisani, haijalishi anayo heshima gani. Kumbuka YESU wa Nazareti ndiye mwenye heshima kuliko mtumishi yeyote ulimwenguni hapa, ila yeye alipokufa alizikwa mbali na kanisa, mpango wa ysu wa kuzimu ni kuzika madhabahuni ili kuharibu nyumba ya ibada, na nyumba hiyo huwa ni eneo la mizimu, maana huyo mtu hatafufuka, na jengo hilo hizo ibada mnazoenda kushiriki ni mpango wa yesu wa kuzimu. Mnapoenda kushirikiana na mizimu, na nyie mnaunganishwa bila kujua, haijalishi amezikwa kwa jina la yesu. Huo sio mpango wa YESU wa Nazareti. Kimwili tu, mwanadamu hapendi kwenda kaburini, maana mtu akishakufa basi, na kaburini ni mahali pa mfu, na kama kwenye kanisa mfu amezikwa hapo, tujue mahali hapo ni madhabahu mfu na wote mnaosali hapo mmekufa. Huu ndio ukweli, fungukeni mpone, haya ninayokuambia, usiniangalie kama mimi Hebron, haya siyaongezi wala sipunguzi hata moja, nakufikishia kama vile Yohana mbatizaji alivyotumwa kubatiza kwa maji mengi bila kubadilisha, na mimi haya ndiyo niliyoambiwa niyahubiri ulimwengu mzima siku zote, na ayakayejaribu hataishi asema bwana, kama unabisha wew jaribi. Jambo linguine inawezekana wewe ni muumini na unayaona matendao machafu kanisani, na ukimweleza mtumishi anayakataa, japo anajua ni kweli, mahali hapo ujue anaonozwa na ysu wa uongo! Maana kama ndani yake angekuwa ana YESU wa kweli, angekusikiliza, ila hawezi kukusikiliza sababu hampo njia moja nay eye. Yeye yupo katika nja ya yesu wa uongo. Mahali hapo sio salama. Mwenye kusikia na kuelewa na aelewe.
11. Ndugu msomaji, nikuulize swali, Je, unajua ule mwisho wa ulimwengu huu atakuja YESU wa Nazareti kuwachukua walw walio wake, sasa ndugu msomaji kama wewe upo chini ya yesu wa uongo, unategemea akuchukueje? YESU wa kwali atakuchukua uende kwake? Jibu ni hapana. Laiti tungeona jinsi watu maelfu kila siku wanakufa na kwenda kwa yesu wa kuzimu, yaani kuna siku moja katika nchi hii ya Tanzania siku nzima eote wanakwenda kuzimu, wote waliokata roho kwa kufa; inatisha na kuna siku moja katika vifo vya waliokata roho ni watu 21 tu walienda paradiso. Wengi wameenda kuzimu, muwe makini msitishwe tena na miujiza ya kipepo, huo ni ujanja wa shetani kuwateka, ila wajanja wamefunguka. Zaidi hata katika ulimwengu huu kama YESU mweyewe alikataa asiitwe mwema (mtakatifu), akasema hakuna aliye mwema, ni MUNGU tu, leo hii unasikia mtu au wa tu wanajiita mama mtakatifu, dada mtakatifu, baba mtakatifu, je, hii ni sawa? Jibu siyo. Na yesu wa kuzimu, wale anaowaongoza, huwa hayo majina aliyoyakataa YESU wa Nazareti, kataa, mmeabiwa ni udaganyifu, hata kibinadamu tunajua yupo ROHO MTAKATIFU andyetoka kwa MUGU MTAKATIFU. Ila yesu wa kuziu hutoa roho chafu na huendeleza machafu kama ilivyo sasa.
12. Yesu wa kuzimu katika kanisa anazo sadaka nyingi sana, sadaka ya YESU wa Nazareti ni fungu la kumi tu na shukurani unayopenda kumpa kwa moyo mweupe. Hizo nyingine zote zimebumiwa na yesu wa uongo ili kukuibia wewe. Yesu wa uono hukusanya madeni na kuwadai waumini ili kulipia madeni na kujengea mahekalu ya yesu wa uongo, na hao wanaosimama kuchangisha au kudai, hao ni manabii wa uongo. YESU wa Nazareti sio masikini wala yeye hafanyi makusanyo kuijenga nyumba yake ya sala. Kama ni yake, hufungua milango ya kuifanya peke yake kwa njia anayoitaka yeye. Alisema msisumbukie mtakula nini, mtavaa nini. Hayo YESU wa Nazareti aliyasema. Je yeye anasema uongo? Ndugu msomaji angalia panavyonuka, kanisa lilivyotekwa na YESU wa uongo 98%. Na kama kanisa linanuka, ina maana na waumini wananuka dhambi na laana au baraka za ysu wa uongo, au kristo wa uongo.
13. Yesu wa uongo huchagua partner watu wenye pesa ili awanyang’anye mali zao na watu wakijua unawafanya partners na YESU wa kweli kumbe ni yesu wa kuzimu huyo. Siku zote partners kanisani hachaguliwi masikini, lazima awe na pesa, je hao wasio na pesa ni takataka? Jibu ni yesu wa kuzimu, ndiye mwenye ubaguzi; ila YESU wa Nazareti watu wote huwa partners wake wote iwe wana pesa au hawana, anawapenda wote. Jambo lingine ndugu msomaji,  ukiona waumini wanamuogopa au kuingiwa na hofu kila wanapomuona badala ya kumfurahia mchungaji wao, ujue huyo aliyepo ndani yake ni yesu wa kuzimu, ndiye anatisha.
Mtume na Nabii Hebron.

[ad_2]