ZIJUE NYIMBO ZINAZOTUMIKA KUMUABUDU SHETANI KUZIMU!!!

[ad_1]

Nilipoonyeshwa kitengo kingine cha shetani niliwaona malaika zake wakimsifu na kumuabudu wakishirikiana na serikali yote ya shetani nyimbo ambazo wao wanasema ni roho mtakatifu wao akiwaingia mapepo ambaye ndiye roho mchafu akiwaingia kwa nguvu wakati wakimsujudia shetani na joka kuu.
Joka kuu huwavuvia nguvu zake ameiga kama vile watu wanavyoshukiwa na ROHO MTAKATIFU wanaanza kunena kwa lugha, na joka kuu huwavuvia nguvu zake na wao huanza kuimba RAP, kama vile huku ulimwenguni watu wanavyoimba miziki ya RAP ni hivyo hivyo, na wanadamu wanaoimba RAP na wenyewe wamevuviwa nguvu kutoka kuzimu wanaanza kufoka foka, na wanapoziimba mnaunganishwa na wakati wa sifa za kuzimu, na asili ya RAP music ni kuzimu na wote wanaoimba nyimbo hizo mapepo ya roho mchafu yanawaingia na kuwapa mafunuo wa miziki hiyo na kuwakamata vijana wa leo. Kama ilivyo sasa badala ya vijana kujazwa nguvu za ROHO MTAKATIFU vijana wengi wanajazwa nguvu za roho mchafu kupitia hizo nyimbo za RAP na kila muimbaji anapewa uwezo wake tofauti na mwenzake kwa jinsi alivyoshukiwa na hiyo nguvu ya roho mchafu.
Mziki wa RAP umebuniwa na kutumwa ulimwenguni ili kuwakamata vijana wasimpokee ROHO MTAKATIFU na shetani anausambaza kwa speed zaidi na hata watu wengine uuita mziki wa kizazi kipya (kwenye ulimwengu wa roho ni mziki wa kizazi cha nyoka) yaani shetani. Madhara ya nyimbo hizi kila mwanamziki anayeimba RAP jina lake lipo katika ufalme wa shetani na anayeimba nyimbo hizo yeye ni agent wa shetani ili kuhakikisha watu hawampokei ROHO MTAKATIFU ili wapone roho zao bali wampokee roho mchafu ili wafe roho zao na matendo ya uovu yazidi kufanywa. RAP ni uovu mtupu na kujitenga na MUNGU, ila kama mlikuwa hamjui eleweni na muwaeleze na wenzenu. Mnapoimba nyimbo hizo mnaunganishwa na kipindi cha kumuabudu shetani na unatekwa bila kujua, ila wapo wanaoimba nyimbo hizo na ni maarufu sana katika ulimwengu huu wao huenda kabisa kuzimu na kupewa hizi nyimbo na lusifa na wengi wao ni wanachama wa freemason.
NOTE:
Kama unataka kupona wacha kuimba miziki yeyote ya kidunia na zaidi utashangaa na makanisani wameanza kuimba nyimbo kwa mitindo ya RAP eti wanasema wanaenda na wakati. Mmepotea na nyie mmeunganishwa na kuzimu na ndiyo maana makanisa mengi shetani ameyatawala, ni sababu ya nyimbo za kidunia wanaiga. Na jambo lingine watumishi waimbaji wanatumia nguvu za giza wengi sana 90%. Wanapokuja kuziimba katika makanisa wanaunganisha makanisa na kuzimu pasipo hata watu kujua. Muwe makini na mumkatae shetani na yeye atawakimbia.
NABII HEBRON.

[ad_2]