Posts / je-unafahamuchama-cha-joka-kuu

18 Dec 2014 • Prophet Hebron
JE UNAFAHAMU CHAMA CHA JOKA KUU KILICHOPO HAPA DUNIANI?

YESU WA NAZARETI wakati akiniandaa na kunifundisha kuhusu kazi yake na jinsi ya kuifanya au mwongozo wake yeye, akinifundisha mambo mengi sana mengine hayo yatabakia kama ni yangu binafsi kwa utukufu wa MUNGU. Alinionyesha chama cha joka kuu alichokianzisha yeye na kikaja duniani na akapata wanadamu, wao wakawa katika hicho chama na lengo la joka kuu kukianzisha hicho chama ni kuipindua ulimwengu ambao MUNGU aliiumba na akaweka viumbe na vitu vyake ili vimtukuze yeye tu. Alichokifanya joka kuu yeye alileta roho zake na akawatumia wanadamu na hata sasa hizo roho zimejaa katika nchi mbali mbali, chama cha joka kuu ambacho ndicho chama kikubwa na anakimiliki yeye peke yake, chama hicho kinaitwa illuminati party.

Sasa muelewe watu wote wa mataifa yote chama hiki kina kila kitengo ikiwemo hata kitengo cha makanisa na hata sasa wapo wahubiri maarufu katika ulimwengu huu ambao watu wanafikiri ni wahubiri maarufu kutoka kwa MUNGU na kumbe ni wahubiri maarufu wa kutoka kwa joka kuu. Na hawa wahubiri walipewa uwezo mkubwa wa pesa, miujiza na mengineyo ili watumike kuwaangamiza wanadamu, mfano ingia google search illuminati pastors member, iwe ni kwa bara mfano bara la Afrika, America, Europe, Asia na kwingineko utaona majina yao. Sasa hawa mimi nilishaelezwa na YESU akaniambia hao ni adui zake, sasa na wewe msomaji ufunguke ufahamu kama YESU anasema ni adui zake na ni adui wa MUNGU, je hauoni na wao wanawatengenezea watoto wa MUNGU mazingira ili wawe nao ni adui wa YESU pasipo watu kujijua.

Umshukuru YESU aliyenijulisha mimi Nabii Hebron na sasa ninawajulisha watu wote ili mpone na mkajitenge nao. Hata kama katika kanisa unalo Sali pastor wako hayupo katika list hiyo ila dhehebu lipo katika chama hicho au Askofu, Nabii, Mtume, Mwalimu, Mwinjilisti uelewe yeye ameshaliunganisha kanisa na chama cha joka kuu. Chunguza madhehebu, ukiyakuta katika list ya illuminati wewe usipoteze muda. Kimbia ili upone roho yako n usiwe mwana chama wa joka kuu. Najua watoto wa MUNGU hawampendi joka kuu ila wale waasisi na viongozi wanampenda joka kuu na sasa wapo kuiendeleza hiyo kazi ya joka kuu. Na kama umeshajua hivyo je nikuulize ni ibada ngapi umeshiriki na joka kuu? Au ni miaka mingapi? Ila sasa umshukuru MUNGU. Ulimwengu ulimgeuka MUNGU 98%, amenituma YESU niupindue ufalme wa shetani na baba yake ambaye ni joka kuu na kazi inaendelea vizuri sana. Ni lazima ufalme wa shetani uangamie katika jina la YESU WA NAZARETI.

Pia hata wanachama wake na wao watengane na baba yao joka kuu katika kuangamizwa na MUNGU, huo ndio uhalali na mtayaona na myaonapo msishangae, ni YESU WA NAZARETI yupo kazini. Chama hiki kimeyashikilia makanisa mengi na kama kimeyashikilia hayo makanisa basi ni dhahiri kabisa hayo ni makanisa ya joka kuu, na yesu wa kuzimu na mpinga kristo. Mpaka hapo unazidi kupata picha wewe chunguza madhehebu zote katika ulimwengu huu ya kila dini, yale utakayoyakuta utakuwa unapata jibu je upo katika kanisa alilolijenga YESU au alilolijenga joka kuu, na unaposali katika kanisa ambalo lipo katika chama cha illuminati uelewe umemezwa, upo katika tumbo la joka kuu katika ulimwengu wa roho. Na ndiyo sababu ili umezwe na joka kuu ni lazima usiokoke, ubatizwe ubatizo wa maji ya kikombe, ubarikiwe ukiwa mtu mzima, ubatizwe kwa jina la mchungaji na ubatizwe katika kisima, kanisa lazima lifanye biashara na kuwa na mabenki na kuchagua partners wawe wanasupport hiyo huduma. Lengo la chama hicho ni kuwakusanya wanadamu na kuwaingiza katika ufalme wa joka kuu wasiende mbinguni ili wakachomwe na yeye katika ule mwisho wa ulimwengu katika moto wa milele wa jehanamu.

Sasa enyi mataifa yote je niwaulize mnapenda kwenda katika ziwa la moto? Jibu ni uamuzi unao wewe, na wengine ni viongozi mbali mbali lakini nao wapo katika chama cha joka kuu, na kama wapo katika chama hicho sasa haupati picha 98% kila kitu shetani alishatawala? Ikabakia 2% ya YESU, sasa YESU anaukomboa ulimwengu wake yeye peke yake na watu waliomsaliti anasema atapambana nao yeye mwenyewe ajuavyo yeye. MUNGU amekasirika sana, watu wameamua kuwa wana chama wa shetani, wamemkataa MUNGU, basi kama ilivyo aliyopanga MUNGU kwa ajili ya shetani yatawahusu na hao waliopo chini yake. Najua wengi hamjui sasa tubu wewe unayeabudu katika madhehebu yaliyo kaatika chama cha shetani na haukujua, utubu na ujitoe huko kabisa.

Sema BWANA YESU naomba unisamehe dhambi zangu zote, uniandike katika kitabu chako cha uzima wa milele, najitenga na chama cha joka kuu katika jina la YESU. Naja kwako YESU WA NAZARETI unishike mkono, uniongoze wewe nisipotee tena. Hata  nikikosa kanisa la kweli nilinde huku nilipo na uniongoze kwa roho wako mtakatifu milele, Amen.

NOTE:

1.     Chunguza dhehebu lako.
2.     Chunguza kiongozi wako, iwe ni katika kanisa au nchi.
3.     Chunguza matajiri katika ulimwengu huu wale maarufu.
4.     Chunguza kila sekta utaona ni chama cha joka kuu linashikilia na hata katika miziki.
Usiogope hiki ni chama cha siri sana na kimejificha mambo yake hayajulikani na watu sababu yangejulikana watu wangewakimbia, wakabakia viongozi wa dini ambazo wamejiunga huko, msidanganyike ulimwengu wote. YESU hashirikiani na chama cha illuminati wala chama chochote katika ulimwengu huu. Sasa mpone. Zaidi karibu katika kanisa la YESU NI BWANA NA MWOKOI WA MATAIFA YOTE Arusha, Tanzania. Na usome vitabu vya Nabii Hebron, toleo la kwanza na toleo la 16 na vinginevyo vipo katika blog www.prophethebron.blogspot.com au ingia katika website www.prophethebron.org.

Nawafunika kwa damu ya YESU ila wachawi nawachoma kwa damu ya YESU WA NAZARETI.


NABII HEBRON.
Previous Post
Next Post