PEPO SADAKA

[ad_1]


Ndugu msomaji wa makala ya Nabii Hebron, nakusalimu kwa jina la YESU WA NAZARETI aliye hai na sasa yupo mbinguni kwa BABA yake katika kiti cha enzi. Leo, nitakufundisha somo kuhusu pepo sadaka. Natumaini hili ni jambo jipya katika ulimwengu huu ambalo halijulikani na mwanadamu na hata wengine wakisikia nasema pepo sadaka watashangaa.
Sadaka ni asante ambayo mtu au watu hutoa kwa MUNGU aliye hai au kwa miungu, mfano matambiko yote yanayofanywa hizo ni sadaka za miungu au mashetani ambazo wanadamu wanamtolea shetani. Ila katika somo hili la PEPO SADAKA nita base zaidi katika pepo sadaka; asili yake, hasara zake kwa kanisa na wote wanaotoa sadaka zao kwa pepo sadaka.
Pepo sadaka ni roho kamili ya shetani ambayo ameituma kwa wanadamu na kwa watumishi na kwa kanisa ili ashukuriwe yeye na sadaka za wanadamu pasipo hata wana wa MUNGU kujua. Japo wapo watumishi wengi sana wanajua ndani yao wanayo mapepo sadaka. Mapepo sadaka hukaa kwa watumishi na kuwaibia waumini pesa zao kwa njia ya sadaka, na watu wanapozitoa hizo sadaka ule uthamani wa pesa zao zinachukuliwa na freemason katika ulimwengu wa roho, na maisha ya watu huendelea kuporomoka japo ni wakristo na wanatoa sadaka kanisani hata na mafungu yao ya kumi. Ila muumini utaona mambo yako hayaendi ujue sadaka zako zimechukuliwa na pepo sadaka na uthamani wake umechukuliwa na freemason, wewe umebakia kusota na mateso tu.
YESU alipokuwa hapa duniani alisema kuipenda pesa ndiyo shina la mabaya, alikuwa anamaanisha ni kwa watumishi na kanisa, yeye YESU alikuwa anaona mbali, yatakayo tokea katika kanisa na kutekwa na shetani na ndivyo ilivyo tokea, 98% katika ulimwengu wote siyo kanisa lake analoliongoza yeye haijalishi linaitwa kwa jina lake.
Ø NAMNA YA KULIJUA PEPO SADAKA
Ø MAHALI AU KWA MTUMISHI MWENYE PEPO SADAKA
Ø KANISA LENYE PEPO LA SADAKA
Pepo sadaka hauliwezi kulijua kwa sura yake, bali utalijua kwa tabia zake, maana ni roho ya shetani inayokaa ndani ya mtumishi na mtumishi huisambaza katika kanisa lake na kuwatawala waumini na wakishawateka waumini fahamu pia. Sasa ndipo mchungaji na yeye anaingiwa na roho ya tamaa za pesa na kuifanya nyumba ya MUNGU ni mahali pa michango tu na ibada zote wimbo wake wote ni sadaka tu kuitaja badala ya rehema na kufundisha mambo mengine ya utakatifu.
Tunajua kila mtu anapoenda kanisani kuna muda wa kutoa sadaka na sadaka ni hiari yako ukipenda mwenyewe. Sasa embu jiulize kwa nini mahubiri kila siku ni habari ya sadaka tu na zipo nyingi? Jibu, uelewe sasa aliyopo ndani ya mtumishi huyo au madhabahu hiyo ni pepo sadaka au mfilisi ambaye ni roho ya shetani, au harambee, hiyo ni dalili 100% ya pepo sadaka. Huyu pepo ni mfilisi aliyetumwa na ibilisi aibe uthamani wa pesa za watu halafu anaupeleka kwa shetani, hizo pesa zenu anawapatia wale wanaojiunga na freemason, na matokeo yake hali yako inakuwa mbaya zaidi kiuchumi na kiroho.
Sasa ndugu msomaji umepata picha kwa nini sadaka unazotoa sana tena mpaka unafilisika, jibu sasa umelipata. Pesa zako hazikwenda kwa YESU WA NAZARETI. Dalili ya kujua sadaka yako imeenda kwa YESU na inanena mbele za MUNGU, mchunguze mtumishi tabia zake na je anatenda kama YESU? Au ni mwizi?! Soma kitabu cha Nabii Hebron JINSI KANISA LILIVYOMKUFURU ROHO MTAKATIFU, hapo utapata majibu yako kuhusu sadaka yako kama imeibiwa na pepo sadaka au imeenda kwa YESU mbinguni.
Pepo hili likiingia katika kanisa lolote au ndani ya mtumishi yeyote lazima atafanya huduma kwa kudai pesa tofauti na YESU alivyoagiza ‘umepewa bure, toa bure’. Pepo hili ni la uwizi wa mali za watu na  ndilo linalokaa  katika watumishi wenye kuchangisha pesa kanisani, kufanya michango na kufanya biashara na hata kutuma namba ya M-Pesa na akaunti za kuomba pesa kwa ajili eti ya kanisa.
Nikuulize swali, je YESU yeye ni omba omba? Ni maskini? Ni mfilisi? Jibu, siyo. Alisema msisumbukie mtakula nini, hii ni kwa watumishi, je sasa hawasumbukii watakula nini? Kama mtumishi anasumbukia atakula nini, atavaa nini? Ajijue yeye hajaitwa na YESU aliyesema neno hilo. Yeye amejiita au anajifanya au ni mtumishi wa mshahara, na YESU ameniambia hao wote ni wezi wala yeye hawajui na hata majina yao alinionyesha hayapo katika listi ya majina ya watumishi wake. Akaniambia, waeleze watu waujue ukweli na wanijue mimi. Watumishi  wa jinsi hiyo hao wote wameunganishwa na freemason na ndiyo maana roho ya unyang’anyi unafanya kazi ndani yao ili kuzidi kujenga ufalme wa shetani kama ilivyo sasa. Watu wanaona makanisa ni mengi ila siyo ya kweli ni ya uongo zinaongozwa na mtandao wa freemason katika ulimwengu wa roho na ni mali ya shetani 100%.
Na hii watu walipigwa upofu, roho inapoingia ndani ya kanisa, hii inaitwa mfilisi na siyo roho ya MUNGU, na pia roho hii ya pepo la sadaka huwachagua wale wenye kauwezo uwezo katika kanisa na kuwaita partners. Nawaambia partners wote katika dunia hii YESU WA NAZARETI na serikali yake hawawatambui kabisa maana pesa hizo mnanyang’anywa kwa njia ya kuambiwa nimewatuma mimi YESU, NI UONGO.
Mtumishi anayechagua partners huyo ndani yake analo pepo sadaka (pepo mnyang’anyi) na nafsi yake imeshikiliwa na freemason wanamuongoza ili kuwaibia watu mali zao na kuzipeleka katika ufalme wa shetani, na ndiyo maana fuatilia maisha ya partners ni mateso, madeni, vifungo na kufilisika. Funguka utoke huko na hata usishiriki mahali palipo kinyume na Neno la MUNGU.
Jambo lingine ni nadhiri (hii ni ahadi ya mtu na MUNGU peke yake na siyo mchungaji ajue). Sasa hili pepo sadaka linafanya kazi ndani ya mtumishi na kukuambia uahidi utatoa pesa ngapi na uandike jina, halafu mtumishi anakufuatilia anakuambia hauwezi kufanikiwa mpaka utoe nadhiri uliyomuahidi MUNGU. Wana wa MUNGU mambo yameharibika katika kanisa na roho ya shetani 98% ndiyo inayofanya kazi na siyo ya MUNGU.
Nadhiri ikishajulikana na mtumishi hiyo siyo nadhiri tena. Ila pepo sadaka neno hili la nadhiri kuwanyang’anya pesa na vitu vyenu pasipo kujua. Ila leo nakueleza nadhiri zote usitoe tena ambazo uliahidi na ukatengenezewa mazingira ili ujiingize katika mtego, huo  ni uwizi wa pepo sadaka, nakueleza kwa jina la YESU WA NAZARETI aliye hai, watu wote wa dunia hii, nadhiri hizo ni za uongo, usilipe tena. Kanisa halijaletwa na YESU kuja kukusanya madeni au kuwajengea mitego ya sadaka na ahadi (au sadaka pepo).
Mfunguke fahamu watu wote YESU amechukia sana, hasa hii sadaka ya ahadi (hii ni sadaka pepo au mfilisi). Sadaka zote hizo hazina nafasi yake mbinguni, sasa kama hazipo, zipo wapi? Jibu, kuzimu. Hautabarikiwa utabakia na baraka za shetani nuksi, balaa, mikosi. Jichunguze kama umezitoaga, jibu unalo mwenyewe.
KANISA LENYE PEPO SADAKA (MFILISI AU MNYANG’ANYI)
·        Sadaka zipo zenye majina mengi tofauti na sadaka ya fungu la kumi na shukurani, hizi ndizo za kweli. Hizo nyingine zote ni sadaka za pepo au mapepo na zimeenda kwa mapepo na ndizo wanazopewa watu wanaojiunga na freemason.
·        Ili umuone mtumishi lazima ulipe pesa ndio akupe appointment.
·        Mtumishi akija kanisani akiingia tu, watu humpokea kwa kumtupia sadaka mpaka miguuni. Na pia katika ibada husimama na kukusanya pesa za sadaka mwenyewe, eti watu wanampelekea mkononi badala ya wao kuweka katika chombo cha sadaka wakati wa kutoa sadaka, ila nawaeleza mjue maana wengi hamjui. Anafanya hivyo maana ni lazima afanye hayo, ni maagano ya freemason na ni lazima. Sasa ona jinsi watu walivyoibiwa vitu vyao na maisha yao wakijua wanamtolea YESU aliye hai kumbe ni shetani. Na hii inakupa picha halisi ya kuwa shetani ndiye mwenye majengo ya kanisa na MUNGU aliye hai hana kabisa, yote yametawaliwa na shetani.
·        Huduma yeyote unayokuta unaambiwa toa sadaka kiwango fulani na uandike jina lako, halafu eti wakaipeleke kwenye maombi kwa MUNGU halafu akitoa kibali ndio utaambiwa umekubaliwa umuone au usafiri uende katika nchi yake umuone, hao ni waizi. Watu wengi wameibiwa pesa zao wakatoa (dolla) USD 200 kama sadaka. Sasa cha ajabu ujue ni matapeli na siyo watumishi wa MUNGU wa kweli, utashangaa watu wanapewa majibu eti baada ya maombi waliyofanya na MUNGU, MUNGU amekataa asimuone. Sasa kama amekataa eti huyo MUNGU basi arudishe na pesa ya mtu huyo. Haiwezekani MUNGU wa kweli akukatae halafu aipokee sadaka yako, hata sadaka yako haipokei. Tazama sadaka ya Kaini hakuipokea (watumishi wa jinsi hii ni kiungo cha freemason na wanaongozwa na mapepo sadaka au unyang’anyi).
NOTE:
Usishiri kutoa pasipo kujifunza na ROHO MTAKATIFU akuongoze.

NABII HEBRON.

[ad_2]