SEMINA ZA NDOA KATIKA MAKANISA YA LEO (ALL OVER THE WORLD) 70% NI MAFUNDISHO YA MAMA WA MAKAHABA (YEZEBELI) (UMALAYA)

[ad_1]

Ndugu msomaji wa makala ya Nabii Hebron, leo nitafundisha na kuelezea kidogo tu kuhusu mafundisho ya semina za ndoa zinazofanywa na kanisa la leo katika ulimwengu wote ni mafundisho ya kumchukiza MUNGU na siyo ya kutoka hata katika Biblia au katika kitabu kitakatifu na cha ajabu mafundisho hayo ya uovu yanafundishwa na leo wanaojiita watumishi wa MUNGU, wakiwa wameshapotezwa na huyu mama wa makahaba ambaye kazi yake ni kuwaua watumishi na wanandoa kiroho, na kwa lugha nyingine hivi ndivyo kanisa lilivyotekwa na shetani na maajenti wake na kuwatumikisha watumishi kufundisha upuuzi au uovu na kuziharibu ndoa kabisa badala ya kuzitengeneza ili zipone, na shetani hapendi ndoa zipone, anajua ndoa zikipona tu watu na familia zitapona, nchi zitapona, mataifa yatapona na yatamrejea MUNGU na kujua atakavyo yeye, ambaye ndiye muasisi wa ndoa, ila sasa imekuwa ni kinyume na mafundisho ya MUNGU yamewekwa au kutupiliwa mbali na kupuuzwa bila ya wanandoa kujua. 

Ukisoma 2Falme 9:34-37, alipoingia akala na kunywa kisha akasema haya mwangalieni mwanamke huyu aliyelaaniwa, akamzike kwa maana ni binti mfalme, wakaenda ili kumzika lakini hawakuona kitu ila kifuvu cha kichwa chake na miguu yake na vitanga vya mikono yake, basi wakarudi wakampasha habari. Akasema, hili ndilo Neno la BWANA alilolinena kwa kinywa cha mtumishi wake Eliya, mtishbi, kusema, katika kiwanja cha Yezreeli mbwa wataila nyama ya Yezebeli. Na mzoga wa Yezebeli utakuwa kama mavi juu ya uso wa mashamba, katika kiwanja cha Yezreeli hata wasipate kusema huyu ni Yezebeli. 

Ndani ya Yezebeli, mwanamke huyu ndani yake ni ile roho ya Yezebeli ndiyo iliyokuwepo ambayo imeandikwa katika kitabu cha Ufunuo 17:4-5, na mwanamke Yule alikuwa amevikwa nguo ya rangi ya zambarau, na nyekundu, amepambwa kwa dhahabu na kito cha thamani na huku naye alikuwa na kikombe cha dhahabu mkononi mwake, kilichojawa na machukizo, na machafu ya uasherati, wake na katika kipaji chake cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa la siri BABELI, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI. 

Ndugu msomaji wa makala ya Nabii Hebron, mpaka sasa natumaini unazidi kumuelewa huyu mama wa makahaba ni nani? Ila utaendelea kusoma katika Biblia yako mwenyewe mistari ya (6-12) utaelewa zaidi. Yezebeli huyu ndiye muasisi wa uasherati na uasherati huu upo katika mkono wake ambao yeye huwagawia wanadamu ili watende uchafu usiofaa katika tendo la ndoa, pia na kulifanya au kuliharibu lisiwe ni ndoa takatifu bali ziwe ni ndoa chafu na machukizo mbele za MUNGU pasipo hata wanandoa kujua au kupenda, ila nitakueleza ili upate kupona ndoa yako isiwe ni ya machukizo mbele za MUNGU, na wanaoifanya ndoa hiyo iwe chafu mbele za MUNGU ni jinsi unavyoyapokea mafundisho ya machukizo kama nitakavyoelezea na asili yake yametokea wapi. 

Kama nilivyoelezea mwanzoni kuwa semina za ndoa za siku za leo zinafundisha mafundisho ya kikahaba kuhusu tendo la ndoa 70% na ndiyo maana ndoa zinaangamia na MUNGU kuziacha maana wanandoa wanafundishwa na watumishi mafundisho ya kikahaba ambayo asili yake ni ya huyu mama wa makahaba ndiye anaye yatoa mafundisho hayo na siyo MUNGU aliye waumba wanadamu. Kwa mfano , yafuatayo ni mafundisho ya kikahaba . 

1. Staili zote za kufanya tendo la ndoa tofauti na wana ndoa kukutana mbele kwa mbele, hizo zote ni machukizo kwa MUNGU, hizo staili nyingine zote ni za wanyama, na za mapepo, mfano wana ndoa wengi na wengine siyo hata wanandoa hutumia miili yao kinyume na maumbile bila kujua ni machukizo kwa MUNGU na wengine wanajua. Neno la MUNGU linasema , ndoa na ziheshimiwe je, huku ndiko kuheshimiwa kwa ndoa na zaidi eti hao wanaojiita watumishi 70% ndiyo mafundisho wanayo yafundisha, je, ndoa zitapona? Jibu haziponi zinazidi kuangamia na kupelekwa pa baya ni hao wanafundisha unyago, Naita ni unyago maana siyo semina ya ndoa za mafundisho ya MUNGU. Ila hutumia jina la YESU ili watu waende katika unyago, wanachofundishwa ni staili za ngono za uzinzi na anayezifundisha ndani yake ipo roho ya Yesebeli ndiyo inayofanya kazi ya kuuwa ndoa hizo na ziwe laana na mpaka ndoa nyingi zimelaaniwa sababu ya kutenda tendo la ndoa kama mbwa wafanyavyo, (dog stail) Kulamba viungo vya siri kwa wanandoa haya ni machukizo na asili yake ni Yesebeli na MUNGU huzuia Baraka za ndoa hizo, MUNGU siyo mjinga aliyekupa mdomo, na viungo vya siri vyenyewe kwa vyenyewe. 

Ile kutumia kiungo tofauti na MUNGU alivyokipangia kazi yake ni dhambi tupu. Mfano mdomo umepitishwa na MUNGU kwa ajili ya kula chakula, kuongea, na kumsifu yeye tu, sasa shetani amewateka fahamu hao watumishi, wakaanza kumsaidia shetani kazi kufundisha wanandoa kutumia viungo vyao kinyume na alivyopanga mwenyezi MUNGU . Sasa hivi hata wewe unayesoma makala haya 99% ni bahati kama hajashiriki kufanya machukizo, kama yesebeli kwa kutumia mdomo kunyonya viungo vya siri na wengine kubadilisha mdomo wake ndiyo kiungo cha kike kwa kuwekea kiungo cha kiume mdomoni. Haya yote ni machukizo na anayekufundisha hizo staili za Yesebeli na y eye mwenyewe lazima anazifanya. Na kama watumishi wanafundisha hayo ya Yesebeli je, hao ni watumishi wa YESU au Yesebeli? Jibu ni wa Yesebeli, kimtokacho mtu ndicho kilichoujaza moyo wake, na Yesebeli hukaa ndani ya moyo wa huyo afundishaye hayo machukizo, hasara inakuwa kwako wewe unayeshiriki hizo staili. 

Ndoa yako inaingiliwa na faraka na majini na mapepo, na ndoa kuibiwa uthamani, upendo unapotea, na nguvu za kike na kiume zinapotea, sababu ndoa yenu inakuwa imeshikiliwa na shetani, na zaidi utakuta unafundishwa eti hizo staili ndiyo unamwonyesha mwenzako upendo. Siyo kweli, upendo hukaa katika moyo  haungalii hayo. Ila wenye majini mfano maimuna kwa wanawake, akiwa nalo lazima mwanamke afanye staili za kipepo ndio atafika na mwanaume huwa na jini linaloitwa abubakari, na y eye mpaka afanye staili za kipepo za Yesebeli ndio atafika. Na zaidi wote wenye majini hayo hupendelea kufanya staili za machukizo ya Yezebeli sababu ndani ya miili yao watoto wa Yesebeli wamekaa. Hizo ni roho wala huwezi kujijua, wanaofanya hivyo wajijue wamemkosea MUNGU na ndoa zao siyo Baraka kwa MUNGU tena ni laana, sasa cha ajabu staili hizi ndizo katika semina za ndoa watu wanafundishwa, nikuulize swali je ndoa zinajengwa au zinabomolewa? Jibu unalo. 

Na pia ujue kuna mavazi ya yezebeli na cha ajabu watu wanafundishwa eti kwa jina la YESU yaani kanisa wanawaacha wavae BIKINI. Hizi ni chupi za mapepo, wanazovaaga, sasa wametengeneza ili wanawake waliopo hapa duniani mara wakizivaa tu, na wao wanakuwa wanawake wa kipepo na mapepo ya kiume huwatafuta katika ndoto na kuzini nao kama wake zao. 

Funguka akili usikubali hayo mafundisho ni ya Yezebeli 100% hayafai kupatia wanadamu kabisa. Nilishangaa sana watu wengi wenye ndoa katika kuwafungua katika matatizo ya ndoa, unakuta ni msingi wa mafundisho ya Yezebeli. Tena wanafundishwa na watumishi, ni ajabu na ni aibu. Ole wao jehanamu inawasubiri, mnatumia jina la YESU kufundisha ukahaba na kuutenda kwa waumini makanisani. Na makanisa hayo wanayo shirikishwa mafundisho hayo. Ni makanisa ya Yezebeli na siyo ya YESU wa NAZARETI. Msimchafue YESU kabisa na mkome. Siku ile ya mwisho sijui utamjibu nini. 

NOTE: Staili zote tofauti na wanadamu alivyoumbwa na MUNGU wakutane (na ni staili moja tu ndiyo takatifu.) hizo nyingine zote ni dhambi, ni uchafu , ni za Yezebeli ni za kuharibu ndoa yako na MUNGU kuwaacha na shetani awe ndie kiongozi wa ndoa hiyo. Ndiyo maana nawaambia 98% kanisa limetekwa limepoteza muelekeo kama ilivyo hivi. Kila mtu awe macho na mafundisho ya uongo yametapakaa makanisani. Ya MUNGU yameachwa, tafuta katika Biblia hakika hamtakuta hizi staili zimeruhusiwa na MUNGU. Bali utaona ni za shetani na wanadamu ndio baadhi yao wamefundishwa katika mapango ya kiroho. (siyo kanisa) 

NABII HEBRON


[ad_2]