Close

WATUMISHI WA MAKANISA YA LEO 98% NI WATOZA USHURU.


(ALL OVER THE WORLD)
Ndugu msomaji ya makala ya Nabii Hebron, natumaini hautakuwa na ubishi kabisa kuhusu watumishi wa makanisa, iwe Nabii, Mtume, Mchungaji, Mwinjilisti, Mwalimu na watenda kazi wameacha kazi ya YESU WA NAZARETI ya kueneza injili ya kweli na kutoa bila malipo sawa sawa na mwenye kanisa ambaye ni YESU WA NAZARETI alivyoagiza. (Mathayo 10:8 mmepewa bure, toeni bure) hii inamaanisha kuwa mpango wa MUNGU kuwapona wanadamu haiitaji ulipie pesa yeyote kama vile unavyolipia hospitali maana yeye ni MUNGU na vyote ni vyake.
     
Ukisoma katika kitabu cha Mathayo 9:9-13 YESU  anamuita Mathayo  aache kazi aliyokuwa anaifanya ya utoza ushuru amfuate yeye awe mwanafunzi wake. Huu ni mfano mzuri ambao tulionyeshwa njia na hivyo kabla ya kuwa mtumishi lazima ulikuwa na mambo yako kama Mathayo. YESU alimwambia wacha maana kazi ya kutoza ushuru ni ya Kaisari na ya Kaisari mpe Kaisari na ya MUNGU mpe MUNGU.
Sasa watu wote mfunguke ufahamu ya kuwa sasa hivi kanisa 98% siyo kanisa tena bali ni kitengo cha dini na watumishi baadhi yao cha kukusanyia kodi kwa waumini wakiwadanganya ni sadaka. Nakueleza MUNGU amechukia sana. Nilipokuwa naongea na malaika Gabriel mtumishi wa MUNGU katika habari aliyokuwa ametumwa na MUNGU anieleze ambayo ni siri yangu. Alipomaliza akaniambia rafiki yangu nakupenda sana na sisi sote tunakupenda mbinguni na tunafurahi jinsi unavyomtii MUNGU aliye BABA yetu, sisi tupo na wewe milele. Na malaika huyu ndiye malaika achukuaye roho (ndiye akataye uhai) sasa ogopeni MUNGU na muache uovu, na yeye anawaangalia tu ila akitumwa lazima atende. Akaniambia Hebron MUNGU aliwaita watumishi wachache tu siyo kama inavyoonekana leo hii walivyo wengi. Wengi wamejiita na kujifanya na wengine ni wachawi na wengine ni wafanyakazi wa mishahara tu. Hao wote MUNGU hawatambui wala hayupo nao. Ila katika wachache aliowaita nao wamebakia 2% katika ulimwengu wote, hao 98% ni wachawi, freemason, na ni watoza ushuru wa leo hii.
Niliogopa kujua tena kumbe watumishi sasa hivi mpaka malaika Gabriel anawaona na anawajua wamekuwa ni watoza ushuru. Akanieleza harambee zote na sadaka za ujenzi, ahadi, collection na nyinginezo tofauti na fungu la kumi na shukurani hizo zote hazina mahali pake mbinguni. Huo ni mchomeko wa shetani wa kulifanya kanisa badala ya kuwa nyumba ya sala imekuwa ni nyumba ya watoza ushuru. Waeleze wote wa mataifa yote, hizo sizo sadaka ni ushuru au kodi unayochajiwa na watumishi au tax collectors kama ilivyo hapa duniani kwa MUNGU hakuna kulipa kodi wala yeye siyo mnyang’anyi. Huduma yake ni bure ila ukikuta unaambiwa utoe malipo yeyote yakupewa jina la sadaka hicho ni kiini macho, huo ni ushuru kama walivyofanya mafarisayo na masadukayo enzi zile alipokuwepo YESU hapa duniani. Na walimchukia YESU kwa sababu moja wapo alikataa mambo yao likiwamo la ushuru na ndiyo maana YESU akasema muwe makini na mafarisayo na masadukayo ambao hupita sokoni na kusimama wakiwa na mavazi yao marefu ili watu wawaheshimu.
Ndugu msomaji YESU alimaanisha sokoni siyo masoko ya matunda, nguo, magari au supermarket, anamaanisha watumishi ambao katika makanisa yao watu wawaelewe ya kuwa mahali walipo au hata katika ibada hizo hapo MUNGU hayupo ni sokoni pa wanyang’anyi au watoza ushuru. Na hata hapa ulimwenguni kwa kweli si watu wanawaheshimu sana hawa watumishi wenye tabia za uwizi na kuchafua jina la MUNGU na kuchangisha harambee na kutoa huduma za kiroho mpaka ulipe pesa. Sasa hawa ndio watoza ushuru na YESU watumishi wake yeye hawachaji pesa ndio wakuombee bali watoza ushuru. Sasa wametawala makanisa 98% ulimwengu wote.
MIFANO MIDOGO YA USHURU MAKANISANI
1.   Ili umuone mtumishi kwa appointment unadaiwa pesa (huyo ni mtoza ushuru).
2.   Kuchajiwa ada yeyote katika kanisa (ushuru huo).
3.   Kuchaguliwa kuwa partners (umekuwa wewe ni mlipa ushuru maalum).
4.   Sadaka zote tofauti na fungu la kumi na shukurani, hizo nyingine zote kwa majina yake ni kodi mbali mbali unachajiwa kama vile katika ulimwengu huu unalipa kodi ya serikali mfano mafuta, nauli, vifaa mbali mbali. Hii yote ni mpango wa shetani kuharibu maisha ya wanadamu, waangamie na wafilisike bila ya MUNGU kuwabariki na ndiyo maana wakristo idadi kubwa ni maskini na hata waliomatajiri utakuta wanatumia nguvu za shetani ni washirikina, hii husababishwa na roho ya mfilisi na michango ndani ya makanisa,na watu wakijua wanamtolea MUNGU kumbe siyo ni wanatozwa ushuru na MUNGU hapokei ushuru; ya Kaisari mpe Kaisari na ya MUNGU mpe MUNGU.
NOTE:
Kama wametoa huduma za kiroho mpaka ulipe pesa basi hakuna ujanja wa kukwepa, wao siyo watumishi wa kweli wa MUNGU, hao ni watoza ushuru wanaowaibia watu mali zao kwa kutumia kivuli cha jina la YESU, wakati YESU hana tabia hizo, hao wanamchafua BWANA YESU.
Mfano halisi ulitokea katika nchi ya Tanzania, alitokea mtumishi (Mchungaji) akasema ametoa huduma ya maji ya kikombe eti MUNGU amemwambia achukue (TSH 500) hataki zaidi. Nawaeleza watu wote muwachunguze watumishi maana wengi mnaona mnaongozwa na mtumishi wa kweli kumbe mnaongozwa na watoza ushuru. Mchungaji huyu amemchafua MUNGU na ni muongo anamsingizia MUNGU. Soma Mathayo 10: 7-9. Toa bure huyo ndiye MUNGU. Ila kuchaji pesa hiyo ni roho nyingine ya mtoza ushuru ya kuzimu ndiyo ipo ndani yake. Watu wengi walikwenda kwa mtoza ushuru wakifikiri wamekwenda kwa YESU WA NAZARETI na ndiyo maana hakuna kitu watu wamepata huko zaidi ya vifo na mateso zaidi.
Na katika makanisa 98% katika ulimwengu huu watu wanafikiri wanaenda katika majengo ya makanisa kumbe ni kinyume, wanaenda kwa watoza ushuru. Ndiyo maana mateso na vifungo vinajaa kwa watu sababu watumishi 98% siyo watumishi tena wa YESU bali wamekuwa ni watoza ushuru. Na kwa watoza ushuru hakuna uzima wa milele, bali ni mfilisi na kufa kiroho na kuzubaishwa ukae hapo hapo mpaka akija YESU kuchukua kanisa lake asikukute katika kanisa lake bali upo kwa watoza ushuru na wanyang’anyi. Soma vitabu vya Mafundisho ya Nabii Hebron utapona roho yako na kufunguka. MUNGU amesingiziwa uongo sana kama enzi zile za Adam na Hawa, shetani alichafua jina la MUNGU kwa kumsingizia uongo. Hivyo na watumishi 98% hawana tofauti na shetani wa leo. Ila mwisho unakuja, tubu wacha uwizi na kazi ya utoza ushuru maana hicho ni cha Kaisari siyo cha YESU.
Ni ajabu hata serikali zote katika uliwengu huu zina hofu ya kumchaji MUNGU kodi, mpaka makanisa hawachaji kodi. Sasa cha ajabu hawa wanaojiita ni watumishi, kwa nini wanawachaji watu ushuru? Je ni halali? Na hayo makanisa yote hayapo chini ya serikali ya kila nchi? Je nyie serikali zote hamyajui haya? Ina maana hizi serikali ni MUNGU ndiye anaziongoza, na haya makanisa yanaongozwa  na shetani kupitia watumishi hao watoza ushuru.
Basi kama makanisa baadhi yamekuwa watoza ushuru basi yamekuwa Kaisari na yenyewe yalipe kodi yasimuibie Kaisari yaani hizi serikali. Kila mahali panapofanyiwa michango, au ulipe ada ya kanisa, nawaeleza nilivyoelezwa na MUNGU mwenye ulimwengu huu, hao ni wezi na MUNGU hajawatuma kutoza watu ushuru maana yeye siyo mtoza ushuru. Anawapenda wote mrudieni yeye, wakati wowote atarejea muda wa YESU kurudi ameniambia umefika ila hajui muda wala siku ya kuja. Ishi katika utakatifu, msikubali kutozwa  ushuru kanisani.
NABII HEBRON.